Mwenyekiti wa Bunge ambaye pia ni Mbunge wa Njombe Mjini, Deodatus Mwanyika akiongoza mjadala wa wabunge kuhusu makadirio ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2026-2027 unaoendelea bungeni Dodoma Aprili 9, 2026.
Mbunge wa Njombe Mjini, Deodatus Mwanyika amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuupatia Mkoa wa Njombe miradi mingi ya maendeleo kikiwemo Chuo Kikuu.
Aidha, Mwanyika akichangia hotuba ya Waziri Mkuu bungeni Dodoma Aprili 14, 2026 hajasita kueleza ukweli kwamba bila kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya Itoni - Lusitu mradi wa chuma wa Liganga hautakuwa na maana, kwani unategemea sana barabara hiyo.
Comments