Bodi ya Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) imemteua rasmi Rais wa Klabu ya Young Africans Sports Club, Hersi Said, kuwa balozi wa Kiswahili ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
Mhandisi Hersi atakuwa miongoni mwa mabalozi watatu wa BAKITA, akishirikiana na Salma Kikwete na Jorum Mkumbi,” amesema Consolata Mushi, Katibu Mkuu wa BAKITA.
Tunampongeza Mhandisi Hersi Said kwa heshima hii kubwa, ni uthibitisho wa mchango wake katika kukuza na kuenzi lugha ya Kiswahili.
Tunamtakia mafanikio mema katika jukumu lake jipya la kuitangaza Kiswahili ndani na nje ya nchi.

Comments