|
Meneja wa Kiwanda cha Kutengeneza Kimea cha Kampuni ya Bia Tanzania
(TBL), Vitus Mhusi akiwaonesha baadhi ya waandishi wa habari, jinsi
shayiri inavyoloweshwa tayari kutengeneza kimea cha bia katika mitambo
iliyopo eneo la Pasua, mjini Moshi, Kilimanjaro. Kulia ni Pantaleo
Temba Mwendesha mitambo mwanadamizi wa kiwanda hicho. |
|
Meneja wa Kiwanda cha Kutengeneza Kimea cha Kampuni ya Bia Tanzania
(TBL), Vitus Mhusi akielezea jana kwa waandishi wa habari (hawapo
pichani) sehemi inayotumika kuongoza mitambo ya kutengeneza kimea kwa
kutumia zao la shayiri iliyopo eneo la Pasua, mjini Moshi, Kilimanjaro. |
|
Shayiri ikiwa imeota tayari kutengenezea kimea |
Fundi wa Maabara ya Kiwanda cha Kutengeneza Kimea cha Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL), Antony Mlay akiwa katika mashine ya kupima ubora wa
upishi wa kimea jana katika maabara ya kiwanda hicho kilichopo eneo la
eneo la Pasua, mjini Moshi, Kilimanjaro.
|
Meneja wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya Kaskazini Mashariki, Kasiro Msangi (kushoto), akimkabidhi Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi, Dk.Emmanuel Meagie msaada wa magodoro 100 na vyandarua 100 vyenye thamani ya sh. mil. 6.Hafla hiyo ilifanyika katika hospitali hiyo mjini Moshi jana.
1824 |
Akina mama wanaowauguza watoto wao wakiwa na furaha baada ya kuambiwa kuwa tbl imewapaatia magodoro 100 na vyandarua 100 katika hospitali hiyo ya Mawenzi Mjini Moshi.
Comments