AFIKISHWA POLISI KWA KUUA VYURA WA JIRANI



Bwana mmoja nchini Ujerumani amefikishwa mahakamani siku ya Alhamisi, baada ya kuwapiga risasi na kuwaua vyura wawili wa jirani yake.
Gazeti la Rheinische Post limesema bwana huyo aliwapiga risasi vyura wa jirani yake saa nane usiku.
Mmoja wa vyura hao alifariki papo hapo, na chura mwingine kufariki kesho yake. Taarifa zinasema, majirani hao, wote wana mabwawa ya maji, ingawa mmoja ana vyura wake na mwingine hana. Aidha habari zaidi zinasema, mara nyingi katika msimu wa kuzaliana, vyura hupiga kelele usiku, kama ilivyokuwa katika tukio hilo.
"Nilisikia mlio wa bunduki, na mara moja nikajua kilichotokea," amesema Andreas van Straelen, ambaye vyura wake walipigwa risasi. Alikwenda nje na kukuta vyura wake wakiwa na matundu ya risasi. Alimchukua mmoja wa vyura hao na kumuweka katika friji, kama ushahidi. Mtuhumiwa amegoma kusema lolote kuhusiaa na sakata hilo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.