Bwana mmoja nchini Ujerumani amefikishwa mahakamani siku ya Alhamisi, baada ya kuwapiga risasi na kuwaua vyura wawili wa jirani yake.
Gazeti la Rheinische Post limesema bwana huyo aliwapiga risasi vyura wa jirani yake saa nane usiku.
Mmoja wa vyura hao alifariki papo hapo, na chura mwingine kufariki kesho yake. Taarifa zinasema, majirani hao, wote wana mabwawa ya maji, ingawa mmoja ana vyura wake na mwingine hana. Aidha habari zaidi zinasema, mara nyingi katika msimu wa kuzaliana, vyura hupiga kelele usiku, kama ilivyokuwa katika tukio hilo.
"Nilisikia mlio wa bunduki, na mara moja nikajua kilichotokea," amesema Andreas van Straelen, ambaye vyura wake walipigwa risasi. Alikwenda nje na kukuta vyura wake wakiwa na matundu ya risasi. Alimchukua mmoja wa vyura hao na kumuweka katika friji, kama ushahidi. Mtuhumiwa amegoma kusema lolote kuhusiaa na sakata hilo.
Gazeti la Rheinische Post limesema bwana huyo aliwapiga risasi vyura wa jirani yake saa nane usiku.
Mmoja wa vyura hao alifariki papo hapo, na chura mwingine kufariki kesho yake. Taarifa zinasema, majirani hao, wote wana mabwawa ya maji, ingawa mmoja ana vyura wake na mwingine hana. Aidha habari zaidi zinasema, mara nyingi katika msimu wa kuzaliana, vyura hupiga kelele usiku, kama ilivyokuwa katika tukio hilo.
"Nilisikia mlio wa bunduki, na mara moja nikajua kilichotokea," amesema Andreas van Straelen, ambaye vyura wake walipigwa risasi. Alikwenda nje na kukuta vyura wake wakiwa na matundu ya risasi. Alimchukua mmoja wa vyura hao na kumuweka katika friji, kama ushahidi. Mtuhumiwa amegoma kusema lolote kuhusiaa na sakata hilo.
Comments