BAA YAFUNGULIWA KINYEMELA GEREZANI

Mamlaka katika gereza moja nchini Mexico wamekuta wafungwa wamefungua baa ndani ya gereza.
Mtandao wa China Daily umesema katika baa hiyo wamekuta vinywaji vikali, bia na hata meza ya kuchezea pool. Polisi wa Ciudad Juarez waligundua baa hiyo siku ya jumatatu katika gereza hilo lililopo katika jimbo la kaskazini la Chihuahua, imesema taarifa kutoka ofisi ya mwendesha mashitaka mkuu.
Walikamata chupa ishirini za vodka, chupa ishirini za tequila na makopo mia mbili ya bia. Polisi pia walikuta bunduki tatu, simu 20 za mkononi, bangi misokoto mia moja na themanini na dozi tisini za dawa za kulevya aina ya heroin. Mkuu wa gereza hilo alifukuzwa kazi siku ya Jumatano, na maafisa wengine wa magereza wanachunguzwa, amesema Jorge Chaires, msemaji wa mwendesha mashitaka wa serikali kwa magereza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

Wasifu wa Kizza Besigye

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA