BAA YAFUNGULIWA KINYEMELA GEREZANI

Mamlaka katika gereza moja nchini Mexico wamekuta wafungwa wamefungua baa ndani ya gereza.
Mtandao wa China Daily umesema katika baa hiyo wamekuta vinywaji vikali, bia na hata meza ya kuchezea pool. Polisi wa Ciudad Juarez waligundua baa hiyo siku ya jumatatu katika gereza hilo lililopo katika jimbo la kaskazini la Chihuahua, imesema taarifa kutoka ofisi ya mwendesha mashitaka mkuu.
Walikamata chupa ishirini za vodka, chupa ishirini za tequila na makopo mia mbili ya bia. Polisi pia walikuta bunduki tatu, simu 20 za mkononi, bangi misokoto mia moja na themanini na dozi tisini za dawa za kulevya aina ya heroin. Mkuu wa gereza hilo alifukuzwa kazi siku ya Jumatano, na maafisa wengine wa magereza wanachunguzwa, amesema Jorge Chaires, msemaji wa mwendesha mashitaka wa serikali kwa magereza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.