Meneja wa Manchester United ya England, Sir Alex Ferguson, amekiri kwamba Barcelona ya Uhispania ndio timu bora zaidi ambayo timu yake imewahi kupambana nayo.
Ferguson amekiri hayo baada ya jana Man U kufungwa magoli 3-1, katika fainali ya klabu bingwa barani Ulaya.
Alisema kwamba vijana wake walipumbazwa na pasi za Barcelona, na kamwe hawakuweza kumzuia Messi, na baada ya Wayne Rooney kusawazisha katika kipindi cha kwanza, walitazamia wataweza kufanya vyema katika kipindi cha pili, lakini hayo hayakuwezekana.
Ushindi wa Klabu ya Barcelona ulisherehekewa sehemu mbali mbali duniani ambako mashabiki wa klabu hiyo waliburudika huku wale wa Manchester wakishindwa kuamini walichokishuhudia.
Kauli ya Kocha Mkuu wa Manchester United Sir Alex Ferguson kuwa Barcelona waliwaduwaza na kuwakubali kuwa Barcelona ni Timu Bora Duniani kwa sasa, iliungwa mkono na mashabiki wengi wa klabu hiyo.
Comments