UCHAGUZI WA VIONGOZI WA VYAMA VYA

1. Kamati inawataka wanachama wote wa TFF kwa ngazi zote kukamilisha uteuzi wa wajumbe wa Kamati za Uchaguzi kabla ya tarehe 31 Mei 2011 kama yalivyo maelekezo ya TFF kwa wanachama wake yaliyotolewa mwanzoni mwa mwezi Aprili 2011. 2. Kamati ya Uchaguzi ya TFF inavitaka vyama vya mpira wa miguu vya wilaya ambavyo muda wa ukomo wa madaraka ya uongozi umekwisha/umekwishapita vianze mara moja mchakato wa uchaguzi. Vyama hivyo vinaagizwa kushirikiana na Kamati za Uchaguzi za vyama vya mpira wa miguu vya Mikoa kuhakikisha kuwa vinafanya uchaguzi kabla ya tarehe 31/07/2011, kwa mujibu wa maagizo yaliyotolewa na TFF mwezi Aprili 2011, na vifanye hivyo kwa kufuata Katiba zinazoendana na Katiba ya mfano ya TFF na kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF. KAMATI YA UCHAGUZI -TFF

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.