WEZI WAIBA NYUKI

Maelfu kadhaa wa nyuki, waliokuwa wakifungwa katika mradi wa mamilioni ya dola wa kitafidi wameibiwa katika chuo kikuu kimoja hapa Uingereza.
Nyuki
Polisi katika eneo la Tayside la Scotland wametoa wito siku ya Jumanne kuomba wananchi kutoa tarifa kuhusu mizinga minne ya nyuki yenye maelfu ya nyuki weusi walioibwa kutoka chuo cha kitabibu mjini Dunde. "Wizi huu utatatiza sana utafiti wetu," amesema Dokta Chris Connolly, mkuu wa utafiti huo. Taarifa iliyotolewa imesema nyuki hao ni wa kipekee, na ni rahisi kutambulika iwapo wataonekana wakiuzwa.
Dokta Connolly amesema huenda nyuki hao wameibiwa ili wapelekwe kuzaliana zaidi, au kwenda kuuzwa kwa wataalam wa ufugaji nyuki. "Yeyote aliyefanya hivi, lazima anafahamu mengi kuhusu nyuki" amesema Dokta Connolly.


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.