Maelfu kadhaa wa nyuki, waliokuwa wakifungwa katika mradi wa mamilioni ya dola wa kitafidi wameibiwa katika chuo kikuu kimoja hapa Uingereza.
Nyuki
Polisi katika eneo la Tayside la Scotland wametoa wito siku ya Jumanne kuomba wananchi kutoa tarifa kuhusu mizinga minne ya nyuki yenye maelfu ya nyuki weusi walioibwa kutoka chuo cha kitabibu mjini Dunde. "Wizi huu utatatiza sana utafiti wetu," amesema Dokta Chris Connolly, mkuu wa utafiti huo. Taarifa iliyotolewa imesema nyuki hao ni wa kipekee, na ni rahisi kutambulika iwapo wataonekana wakiuzwa.
Dokta Connolly amesema huenda nyuki hao wameibiwa ili wapelekwe kuzaliana zaidi, au kwenda kuuzwa kwa wataalam wa ufugaji nyuki. "Yeyote aliyefanya hivi, lazima anafahamu mengi kuhusu nyuki" amesema Dokta Connolly.
Nyuki
Polisi katika eneo la Tayside la Scotland wametoa wito siku ya Jumanne kuomba wananchi kutoa tarifa kuhusu mizinga minne ya nyuki yenye maelfu ya nyuki weusi walioibwa kutoka chuo cha kitabibu mjini Dunde. "Wizi huu utatatiza sana utafiti wetu," amesema Dokta Chris Connolly, mkuu wa utafiti huo. Taarifa iliyotolewa imesema nyuki hao ni wa kipekee, na ni rahisi kutambulika iwapo wataonekana wakiuzwa.
Dokta Connolly amesema huenda nyuki hao wameibiwa ili wapelekwe kuzaliana zaidi, au kwenda kuuzwa kwa wataalam wa ufugaji nyuki. "Yeyote aliyefanya hivi, lazima anafahamu mengi kuhusu nyuki" amesema Dokta Connolly.
Comments