CHILUBA AFARIKI DUNIA

Chiluba akiwa na mkewe Regina enzi zake

Rais wa zamani wa Zambia, Frederick Chiluba, amefariki, akiwa na umri wa miaka 68.
Bwana Chiluba amekuwa na ugonjwa moyo kwa miaka kadha.

Rais Chiluba aliiongoza Zambia kwa mwongo mzima katika miaka ya '90, na baada ya kustaafu alishtakiwa kwa sababu ya rushwa.
Frederick Chiluba alipata urais wa Zambia mwaka wa 1991, wakati Afrika inaanza kuingiia katika demokrasi ya vyama vingi.
Kabla ya hapo alikuwa kiongozi wa wafanyakazi.
Aliahidi kuleta mabadiliko lakini alipochukua uongozi Zambia ilikuwa imeshafilisika, naye aliacha rushwa kustawi.
Alipojaribu kujiongezea muhula wa tatu wa madaraka, alipingwa.
Piya alilaumiwa kuwa akipenda maisha ya anasa.
Baada ya kuondoka madarakani mwaka wa 2001, mrithi wake, Levy Mwanawasa, alimshtaki kwa shutuma za rushwa.
Baada ya kesi ya miaka 6 kuhusu ubadhirifu wa mali ya taifa, Frederick Chiluba aliambiwa hakuwa na makosa. .
Lakini katika kesi nyengine iliyofanywa katika mahakama makuu ya London, Chiluba alikutikana na hatia ya kuiba mamilioni ya dola ya fedha za serikali ya Zambia, kwa kutumia akaunti kwenye mabenki ya London.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.