Onesho la mwanamuziki mashuhuri wa muziki wa Jazz, Hugh Masekela (kulia) kutoka Afrika Kusini, limevunjika baada ya mwanamuziki huyo kutotokea jukwaani kwa madai kwamba waandaaji walikuwa hawamlipa malipo yake waliyokubaliana.
Habari tulizozipata kutoka kwa wapenzi wa muziki walioingia katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, Masaki, Dar es Salaam kufurahisha nyoyo zao. walishindwa kupata raha waliyoiripia kwa hela nyingi, baada ya Masekela kutotokea bali walichoambulia ni shoo ya Sauda Kilumanga tu.
Wapenzi wa muziki waliojaa pomoni ukumbini hap, baada ya kuona hivyo walighadhibika na kuanza kulalamika na kutukana ovyo. Wadhamini wakuu wa onesho hilo ni Benki ya Stanbic.
Kamanda wa Matukio itaendelea kuwajulisha mambo mbalimbali yaliyojiri kwenye shoo hiyo na hasa sababu zaidi za uzembe huo.
Habari tulizozipata kutoka kwa wapenzi wa muziki walioingia katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, Masaki, Dar es Salaam kufurahisha nyoyo zao. walishindwa kupata raha waliyoiripia kwa hela nyingi, baada ya Masekela kutotokea bali walichoambulia ni shoo ya Sauda Kilumanga tu.
Wapenzi wa muziki waliojaa pomoni ukumbini hap, baada ya kuona hivyo walighadhibika na kuanza kulalamika na kutukana ovyo. Wadhamini wakuu wa onesho hilo ni Benki ya Stanbic.
Kamanda wa Matukio itaendelea kuwajulisha mambo mbalimbali yaliyojiri kwenye shoo hiyo na hasa sababu zaidi za uzembe huo.
Comments