TFF YATOA KALENDA YA MATUKIO

TFF imetoa kalenda yake ya matukio kwa mwaka 2011/2012 ambapo kipindi cha kwanza cha matayarisho ya msimu kinaanza Juni 1 hadi Agosti 13 mwaka huu. Kipindi cha kwanza cha uhamisho kinaanza Juni 1 hadi Julai 15 ambapo usajili wa kwanza utakuwa Juni 1 hadi Julai 20. Kutangaza wachezaji wa kuachwa/kusitisha mikataba ni kuanzia Juni 1 hadi 21 mwaka huu wakati kupitia majina na kutangaza pingamizi ni kati ya Julai 21-31 mwaka huu. Kipindi cha pili cha uhamisho kitaanza Novemba 1 hadi 20 mwaka huu wakati usajili utaanza Novemba 1 hadi 30 mwaka huu. Ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kutoka Julai 20 mwaka huu. Ngao ya Hisani kwa ajili ya ufunguzi wa msimu kwa mikoa yote itachezwa Agosti 13 mwaka huu wakati mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom utaanza Agosti 20 mwaka huu. TFF tunawaomba wadau wote kuhakikisha wanapata kalenda hii ili waweze kupanga shughuli na mipango yao kwa kuizingatia.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.