Aliyekuwa waziri mkuu wa Libya, Baghdadi Al-Mahmoudi
Rais wa Tunisia, Moncef Marzouki, amesema nchi hiyo haitamuwasilisha kwa mashtaka nchini Libya aliyekuwa waziri mkuu wa Libya, Baghdadi Al-Mahmoudi, bila ya hakikisho kwamba atashtakiwa kwa njia iliyo huru na haki na kwamba atalindwa.
Libya inamsaka Bwana
Al-Mahmoudi kwa tuhuma za kutumia vibaya mamlaka.
Al-Mahmudi alitorokea nchini
Tunisia punde baada ya Kanali Gaddafi kupinduliwa na anameshikiliwa nchini
humo.
Akiwa ziarani mjini Tripoli,
Moncef Marzouki, alisema ni ''haki ya raia wa Libya kumhukumu'' waziri mkuu wao
wa zamani.
Bwana Mahmoudi alikamatwa
nchini Tunisia Septemba mwaka uliopita kwa kuingia nchini humo kinyume cha
sheria.
Makundi ya kutetea haki za
binadamu zimeiomba Tunisia kutomurudisha nyumbani bwana Mahmoundi, yakisema
haki zake za kimsingi zitakiukwa.
Katika hotuba yake mjini
Tripoli, Bwana Marzouki alisema kuwa watu wa Tunisia walitaka kukakisha kwa
1000% kuwa haki ya inatendeka, na kwamba kutakuwa na mahakama huru, kabla ya
bwana Mahmoudi kurudishwa Libya.
Comments