Mkurugenzi Mkuu wa EWURA,Haruna Masebu
SIXTH FLOOR, HARBOURVIEW TOWERS,
SAMORA AVENUE,
P O BOX 72175
DAR ES SALAAM, TANZANIA
TEL:
(+255-22) 2123850; 2123853; 2123854; 2123856; FAX: (+255-22) 2123180
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUHUSU UAMUZI WA BODI YA EWURA JUU YA MAOMBI YA DHARURA YA TANESCO YA KUPANDISHA BEI
YA HUDUMA YA UMEME
Tarehe 9 Novemba 2011, Mamlaka ya Udhibiti wa
Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ilipokea maombi la dharura kutoka Shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO) la kuidhinishiwa ongezeko la bei za huduma ya umeme
kwa wastani wa asilimia 155 ya bei ya sasa. Maombi haya yalisajiliwa Namba TR-E-11-012.
Kulingana
na maombi yaliyowasilishwa, katika mwaka
2010 na 2011 Tanzania
ilikuwa na hali mbaya ya mvua katika maeneo ya mabwawa na hivyo iliathiri
uzalishaji wa umeme. Hii ilisababisha nchi kuwa na upungufu mkubwa wa umeme na
kuathiri sio tu hali ya kifedha ya TANESCO, bali pia na uchumi kwa ujumla wake.
Ili
kumaliza tatizo hilo, TANESCO ilisaini mkataba
na IPTL kuzalisha Megawati 100 kwa kutumia mafuta mazito (HFO); ilisaini
mkataba wa kuuziana umeme (PPA) na Symbion LLC kuzalisha Megawati 112 kutumia
gesi asilia na mafuta; na ilisaini mkataba wa kuuziana umeme (PPA) na Aggreko
kuzalisha Megawati 100 kutumia mafuta ya dizeli.
Vilevile,
TANESCO inatekeleza mradi wake wa Megawati 150 ambao utatumia gesi asilia
pamoja na mafuta (dual fuel plant) na mradi mwingine wa Megawati 70 ambao
utatumia mafuta mazito (HFO). Ukiacha
miradi ya TANESCO ambayo itakamilika mwaka 2012, umeme unaozalishwa kupitia
mikataba tajwa umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la mgao wa umeme
hapa nchini. Hata hivyo, juhudi za kumaliza mgao wa umeme zimeongeza kwa kiasi
kikubwa gharama za uendeshaji za TANESCO.
Katika
kukabiliana na hali hiyo, TANESCO iliwasilisha maombi ya dharura EWURA ikiomba
kuongeza bei za huduma zake kwa 155.
Kulingana
na kifungu Na. 15(1)(3) cha Mwongozo wa Uwasilishaji Maombi ya Bei wa mwaka 2009 (Tariff Application Guidelines of
2009), Waziri mwenye dhamana (kwa hali hii) wa Nishati na Madini, aliwasilisha Hati ya Dharura (Certificate of Urgency) EWURA ili maombi husika yaidhinishwe haraka
na sio kwa utaratibu wa kawaida.
Tarehe
11 Novemba EWURA ilipokea Hati ya Dharura
kutoka kwa Waziri wa Nishati na Madini na hivyo kuanza mchakato wa kupitia maombi
ya TANESCO baada ya kupata maoni ya wadau.
Kulingana
na Kifungu Na.19(2)(b) cha Sheria ya EWURA (Sura 414 ya Sheria za Tanzania), tarehe
2 Desemba 2011, EWURA ilifanya mkutano
jijini Dar es Salaam wa kukusanya maoni ya wadau, kuweka maombi husika katika tovuti
ya EWURA, pamoja na kuwaandikia wadau wachache ili waweze kutoa maoni yao kuhusu
uhalali wa maombi yaliyowasilishwa na TANESCO. Pia maombi tajwa yalitangazwa
katika vyombo vya habari mbalimbali.
Baada
ya kufanya uchambuzi wa maombi yaliyowasilishwa
pamoja na kupata maoni kutoka kwa wadau mbalimbali, Bodi ya Wakurugenzi wa
EWURA ilikutana tarehe 12 Januari 2012 na kufanya uamuzi, pamoja na mambo
mengine:
(a)
Serikali imechangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha kupunguza makali ya
maisha kwa wa Tanzania kwa mosi; kufuta kodi ya mafuta kwenye mitambo, itakuwa
inalipia Sh. bilioni 18 gharama za
mitambo IPTL (Capacity Charges) na kusamehe deni la Sh. bilioni 136 kwa
TANESCO.
(b)
Kutokana na ukokotoaji uliofanywa na EWURA, kwa kuzingatia mzigo ambao
Serikali imeubeba na pia kwa kuzingatia hali ya hewa ambayo inaweza kufanikisha
upatikanaji wa mvua kwa wingi na hivyo kujaza kwenye mabwawa, bei ya umeme itaongezeka
kwa wastani wa asilimia 40.29 kwa
wateja wote isipokuwa wateja wanaotumia uniti 0 – 50 (0 – 50 kWh) kwa mwezi na
ZECO, bei imepunguzwa kwa kwa asilimia 10. Na wafanyakazi wa TANESCO watalipa kama wateja wengine. Bei hizo zitaongezeka kama
inavyoonekana katika Jedwali hapa chini.
(c)
Bei zilizoidhinishwa zitaanza kutumika tarehe 15 January 2012 mpaka
hapo uchambuzi wa kina utakapokamilika na hivyo kutolewa kwa Order nyingine.
Mkurugenzi Mkuu,
Mamlaka ya Udhibiti wa
Huduma ya Nishati na Maji
|
Comments