Jambazi lajipiga risasi kwa wasiwasi

Jambazi mmoja aliyeingia benki kuiba fedha, akiwa na wenzake, alifanikiwa kupora dola takriban elfu kumi na sita, lakini kutokana na wasiwasi akajipiga risasi mweyewe.

Picha za video katika kamera za usalama katika beki moja iliyopo Parana kaskazini, nchini Brazil imeonesha wezi watatu wakiwa na silaha wakiingia katika benki hiyo siku ya Jumatatu.

Kila kitu kilionekana kwenda kama kilivyopangwa, baada ya wezi hao kuwadhibiti walinzi wa benki na kufanikiwa kupora reais elfu thelathini za Brazil, sawa na dola elfu kumi na sita.

Hata hivyo mmoja wa majambazi hao, aliyekuwa mlangoni, alionekana akiwa na hali ya wasiwasi muda wote wakati wizi unaendelea. Mwizi huyo akiwa ameshika bastola mbili alionekana kutokuwa na hali ya utulivu kabisa, na ghafla ulisikika mlio.

Kutaharuki jambazi huyo alikuwa kajipiga risasi mwenyewe mguuni. Picha za CCTV zilionesha jambazi huyo akiondoka eneo la tukio huku akichechemea - OUCH - mguu wake alioujeruhi mwenyewe, huku wenzake wawili wakimtangulia kwa kasi.

Siku iliyofuata, jambazi huyo alikamatwa baada ya kwenda hospitali kutafuta matibabu, katika hospitali iliyo karibu na benki waliofanya wizi wao. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Brazil, majambazi sita walihusika na wizi huo, lakini ni huyo mmoja tu aliyejipiga risasi mwenyewe ndio amekamatwa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA