Jan
14
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akipokea seti ya vyombo vya nyumbani na taa
inayotumia nguvu za jua toka kwa Mkurugenzi wa Home Shopping Centre Bw
Gharib Saidi Mohamed ambaye kampuni yake imejitolea kugawa seti kama
hizo pamoja na taa kwa kila familia 655 zilizohamishiwa Mabwepande
baada ya kuathirika na Mafuriko katika bonge la Msimbazi. Bw Gharib pia
ameahidi kujenga shule ya msingi ya eneo hilo pamoja na kituo cha
polisi.
Rais
Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakitoa heshima zao za
mwisho kwa mwili wa Kamishana wa Magereza Elias Mtige Nkuku, aliyefariki
juzi kabla ya kusafirishwa kwenda kwao mkoani Singida. Hafla hii
imefanyika jana katika bwalo la jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es
salaam.
Rais
Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakitoa heshima zao za
mwisho kwa mwili wa Kanali Pastory Kamugisha wa JWTZ aliyefariki juzi
kabla ya kusafirishwa kwenda kwao mkoani Kagera. Hafla hii imefanyika
jana katika kambi ya jeshi ya Lugalo Jijini Dar es salaam.
Rais
Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete wakioneshwa maeneo ya makazi
mapya ya walioathirika na mafuriko katika bonde la Msimbazi
walipotembelea eneo hilo jana.Picha na IKULU
----
Na Mwandishi Maalumu
Kampuni
ya Home Shopping Centre (HSC) imeahidi kujenga kituo cha polisi,
vyomba 14 vya madarasa ofisi za walimu na chumba cha kulia chakula kwa
ajili ya waathirika wa mafuriko watakaohamia Mabwepande nje ya jiji la
Dar es Salaam.
Mbali
na ahadi hiyo HSC imetoa mifuko 2,000 ya saruji, vyombo vya ndani na
taa za sola kwa familia zote 653 zitakazopatiwa makazi kwenye eneo hilo
Hayo
yalisema leo na Mkurugenzi wa HSC Gharib Said Mohamed mfupi kabla
Kamati ya maafa mkoani hapa kumkabidhi rais Jakaya Kikwete mahema 203
yaliyojengwa na Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS).
Bw
Gharib amesema kwamba shughuli za ujenzi wa vyumba vya madarasa, ofisi
na jengo la kulia chakula vitakamilika katika kipindi cha miezi miwili
kuanzia sasa.
“Kwa
kweli mpaka sasa kwenye saruji, vyombo vya ndani na taa za sola
tumetumia zaidi ya sh milioni 70 kuhusu ahadi ya ujenzi wa kituo cha
polisi na shule mpaka sasa gharama yake hatujaijua hadi
vitakapokamilika,” alisema Bw. Gharib.
Aliwaomba
pia wadau wengine wenye nia ya kuwasaidia wananchi hao kujitokeza kwa
ajili ya kuongeza nguvu kwenye maeneo mengine huku akisisitiza kwamba
jukumu la kusaudua utekelezaji wa majukumu ya serikali kwa wananchi
linawahusu wote.
Awali
rais Kikwete aliitaka kamati ya Maafa inayoshughulikia waathirika hao
kufikiria namna ya kuwapatia viwanja waliokua wapangaji kwenye nyumba
zote zilizobomelewa kwa mafuriko huku akiitaka kamati hiyo kuwa makini
katika ugawaji wa viwanja hivyo
“Msipokua
makini zoezi hili haliishi… mtaendelea kufanya hivi kila siku
watajitokeza pia wasiostahili watakuja kudai viwanja,” alisema rais
Kikwete muda mfupi kabla ya kukabidhiwa na kukagua mahema hayo.
Aidha
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kwa kushirikiana na
Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS) watafanya usafi wa maeneo na
kujenga mahema kabla ya waathirika hao kuhamia Mabwepande.
Comments