Milioni 700 Kutumika Sherehe za Mapinduzi
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Zaidi
ya Shs. Million 700 zinatarajiwa kutumika katika kuadhimisha Sherehe za
miaka 48 ya Mapinduzi Zanzibar ambayo kilele chake kitakuwa Januari 12
Mwezi huu huko katika Uwanja wa Amani Mjini Zanzibar
Akitoa taarifa mbele ya waandishi wa
habari leo huko ofisini kwake Vuga, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa
Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed amesema kuwa fedha hizo ni kwa
makisio tu lakini taarifa kamili ya matumizi hayo itatolewa baada ya
kukamilika kwa sherehe hiyo
Comments