SOKO LA KISASA LA MWANJELWA JIJINI MBEYA KUENDELEA KUWA KITENDAWILI KUKAMILIKA DESEMBA 2012
Mkurugenzi wa jiji la mbeya Juma Idi |
SOKO jipya la Mwanjelwa lililoanza kujengwa Februari
25,2010 ujenzi wa ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2012 ambapo
ujenzi huo ulipaswa kukamilika Agosti 24,2011.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya Juma Iddi
alipokuwa akizungumzia masuala mbalimbali na waandishi wa habari
.
Mkurugenzi huyo amesema kuwa soko hilo likikamilika
liatarajia kuondoa mlundikano wa wafanyabiashara katika masoko ya Sido na Soweto
ambapo tangu juzi wafanyabiashara wa masoko hayo waligoma wakilalamikia kupanda
kwa ushuru kwa zaidi ya asilimia 50.
Katika suala hilo la kupanda kwa gharama za ushuru kutoka
Shilingi 200 kufikia shilingi 300 mpaka 500 kutegemeana na biashara yenyewe,
amesema kuwa gharama hizo zipo kisheria na baraza la madiwani liliridhia lakini
jana juzi na jana wamekaa na wafanyabiashara hao na kufikia makubaliano ya
kulipa Sh 200-300
Amesema licha ya makubaliano hayo, wafanyabiashara
wameendelea kugoma waishinikiza uboreshwaji wa miundombinu katika masoko hayo
likiwemo soko la Sido ambalo ni chafu jambo ambalo ametolea ufafanuzi kuwa Jiji
la Mbeya haliko tayari kufanya hivyo kwasababu masoko hayo si
lasmi.
Ujenzi wa Soko la Kisasa la Mwanjelwa unatarajia kutumia
Sh Bil 10 ambapo ukijumulisha na gharama za kibenki na Kodi ya Ongezeko la
Thamani (VAT), gharama inafikia Sh bilioni 13.
Kampuni ya Tanzania Building Works TBW ya Dar es Salaam
ndiyo inajenga soko hilo.
DESEMBA 2006 Soko la Mwanjelwa jijini Mbeya lililokuwa na
ukubwa wa eka 4.7 liliungua. (PICHA, HABARI KWA HISANI YA BLOGU YA MBEYA YETU)
Comments