Spika Makinda amtembelea Bi. Grace Mongi – Clifton Mtanzania nchini Trinidad and Tobago – aungana na maspika wenzie kutembelea vivutio nchini humo
Mtanzania
aishie nchini Trinidad and Tobago akifanya shughuli zake za
ujasilia mali Bi. Grace Mongi – Clifton akimkaribisha Spika wa
Bunge Mhe. Anne Makinda mara alipomtembelea
Nyumbani kwake nchini Trinidad and Tobago. Mhe. Spika alikuwa nchini
humo kuhudhuria Mkutano wa 21 wa Maspika wa nchi za Jumuiya ya
Madola uliofanyika nchini Trinidad and Tobago
Spika
wa Bunge Mhe. Anne Makinda akifurahia sanamu katika msikiti mkubwa
wa madhehebu ya dini ya KIHINDU uliopo Port of Spain Nchini
Trinidad and Tobago wakati wakitembelea vivutio mbalimbali vya
utalii nchini humo baada ya kumalizika kwa kumtano wa 21 wa Maspika
wa nchi za Jumuiya ya Madola uliofanyika nchini humo.
Spika
wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwa na Maspika wenzie kutembelea
vivutio mbalimbali vya kitalii katika Mji wa Port of Spain katika
visiwa vya Trinidad and Tobago mara baada ya kumalizika kwa kumtano
wa 21 wa Maspika wa nchi za Jumuiya ya Madola uliofanyika nchini
humo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwa na Maspika wenzie kutoka nchi wananchama wa Jumuiya ya Madola wakifuatilia
maelezo ya shughuli za uchimbaji mafuta na gesi asilia kutoka kwa
mwenyekiti wa kampuni ya kuchimba mafuta ya nchi hiyo (hayupo
pichani) mara baada ya kuitembelea kampuni hiyo kujionea shughuli
zake.
Comments