BUNGENI LEO: Mgomo wa madaktari na Sheria ya Bodi ya Mikopo

Asubuhi ya leo Naibu Spika Job Ndugai alitumia kanuni vibaya kuzuia hoja ya dharura bungeni kuhusu mgomo wa madaktari. Kimsingi, sikuwasilisha hoja ila niliomba muongozo wa Spika ili niweze kupatiwa nafasi ya kuwasilisha hoja ya dharura. Kwa kuwa hoja kama hiyo iliwasilishwa juzi na ikaungwa mkono lakini Spika akasema ameshakubaliana na serikali kuwa ingewasilisha kauli. Hata hivyo, jana hakukuwa na kauli ya serikali huku wananchi wakiendelea kupata madhara ya mgomo. Hivyo nikata muongozo kwa kuwa Spika alitumia kanuni ya 49 (2) ambayo kimsingi inatoa mwanya kwa kauli ya serikali kuwasilishwa kwenye wakati atakaoona yeye kuwa na unafaa juu ya jambo linaihusu serikali na lisilozua mjadala. Nilitaka kanuni hiyo isitumike badala yake wabunge tutimize wajibu wa kuisimamia serikali kwa kutumia kanuni ya 47 kuhusu hoja ya dharura. Kwa kuwa ilikuwa muongozo hakukuwa na hitaji la kikanuni la wabunge wengine kuunga mkono lakini akaamua kuilinda serikali kwa kuwa hawakuwa wamejiandaa. Lakini mwishoni ameahidi kuwa kauli ya serikali itatolewa kesho.


Jioni ya leo bunge litajadili Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali na.2 wa mwaka 2011 ambao kwa sehemu kubwa ukiondoa sheria nyingine unahusu marekebisho ya kimsingi katika sheria ya bodi ya mikopo. Ni kwa bahati mbaya kwamba muswada huu umeletwa na hoja ya kusomwa kwa hatua zake zote tatu katika mkutano mmoja hivyo hakutakuwa na muda wa kukusanya maoni ya wadau kwa upana wake. Ni sehemu ndogo sana ya vifungu vya muswada huu ndio inapaswa kukubalika lakini kwa ujumla muswada huu unakwenda kuingiza mambo ambayo tuliyapinga kwa makongamano, migomo na maandamano yakaondolewa wakati sheria husika inatungwa mwaka 2004. Maudhui ya muswada huu yamenifanya nikumbuke makala ambayo niliandika mwezi kama huu lakini mwaka 2007: http://www.chadema.or.tz/makala/makala.php?id=43 Marekebisho haya yanaenda kuweka mazingira mengine ya migogoro katika elimu ya juu nchini kutokana na masuala ya mikopo kwa wanafunzi. Muswada huu ulipaswa kuja bungeni baada ya ripoti ya Tume ya Rais iliyoundwa tarehe 14 Februari 2011 na kukabidhi taarifa yake tarehe 29 Aprili yenye mapendekezo ya jinsi ya kuboresha utaratibu wa sasa wa ugharamiaji, utoaji na urejeshaji wa mikopo ya elimu ya juu kuwekwa wazi kwa bunge na kwa umma ili kufanya marekebisho mapana zaidi ya kimfumo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI