Chisora amzaba kofi Klitschko

Mwanandondi Muingereza ambaye ni mzaliwa wa Zimbabwe, Dereck Chisora amemzaba kofi mpinzani wake Vitali Klistchko kabla ya pambano lao la mjini Munich, Ujerumani, siku ya Jumamosi.

Ripoti zasema Chisora alimrushia kofi Klitschko, ambaye ni bingwa mtetezi wa masumbwi ya uzani wa juu wa tawi la WBC, wakati wa kikao na waandishi wa habari baada ya wote wawili kupimwa uzani wao, tayari kwa pambano la mjini Munich, Ujerumani. Klitschko, ambaye ni raia wa Ukraine, alijizuia kujibu kofi hilo na kukitaja kitendo cha Chisora kama cha kustajabisha.

Chisora, mwenye umri wa miaka 28, amesema licha ya kukosa ujuzi, atampokonya Klitschko taji lake.

Kwa upande wake, Klitschko amejigamba kwamba hakuna upinzani wa kumbabaisha katika harakati za kutetea ubingwa wake.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.