Rais wa Uganda- nchi hiyo itakuwa na uwezo wa kuzalisha mapipa laki 2 kwa siku

Serikali ya Uganda imetia saini makubaliano ya uzalishaji mafuta na kampuni ya Uingereza ya jijini London, Tullow oil.

Mkataba huo unafungua njia kwa uwekezaji wa dola bilioni 10 katika kiwanda cha kusafisha mafuta na bomba la kusafirisha mafuta yasiyosafishwa.

Mkataba huo una thamani ya dola bilioni 2.9 na unamaliza mvutano na serikali ya Uganda kuhusu kodi katika siku zijazo.

Waziri wa mafuta wa Uganda Irene Muloni amesema Tullow imekubali mabadiliko ya vipengele vya serikali vya "kuimarisha" ambavyo vitajumuishwa katika mkataba wa kutetea kampuni dhidi ya hasara iwapo serikali itabadili sheria za kodi.

Msemaji wa Tullow George Cazenove amesema kampuni imeridhika na vifungu hivyo.

"Ni muhimu kukumbuka kuwa maendeleo ya bonde la Ziwa Albert yatakuwa ya muda mrefu kwa maendeleo ya Uganda kwa miaka mingi - kuna mafuta mengi sana pale," Bw Cazanove ameiambia BBC.

"Kutakuwa na kiwanda cha kusafisha mafuta nchini Uganda na bomba pia."

Hazina ya mafuta na kiwanda cha kusafisha vitakuwa vinatosha kukidhi mahitaji ya Uganda, na pia baadhi ya nchi majirani ikiwemo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.