JK aagana na mabalozi wapya wa Tanzania nchini Italia,Uganda na Msumbiji
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ameagana na mabalozi wapya watatu watakaoiwakilisha Tanzania nchi za nje.Mabalozi waliokwenda ikulu kumuaga Rais Kikwete ni pamoja na Dkt.James Msekela anayekwenda Italia, Dkt.Ladislaus Komba anayekwenda Uganda na Mhe.Bi.Shamim Nyanduga anayekwenda Msumbiji. Oichani juu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Balozi Mpya wa Tanzania nchini Italia Dkt.James Msekela ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Comments