JK ATUMA RAMBIRAMBI KIFO CHA MWAKILISHI WA JIMBO LA BUBUBU ZNZ, MAREHEMU MTONDOO


                             UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


Coat of Arms
PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho kuomboleza kifo cha Mwakilishi wa Jimbo la Bububu (CCM) Mheshimiwa Salum Amour Mtondoo.
Hayati Mtondoo alizikwa kijijini kwao Bumbwini, Mkoa wa Kaskazini Unguja jana, Ijumaa, Machi 16, 2012, baada ya kufariki dunia juzi kwa matatizo ya shinikizo la damu, malaria na sukari.
Katika salamu zake kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi, Rais Kikwete amesema kuwa amepokea kwa mshtuko na masikitiko habari za kifo cha Mheshimiwa Mtondoo ambaye alikuwa Mwakilishi wa Wananchi wa Bububu katika Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi.
Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko habari za kifo cha Mheshimiwa Mtondoo. Siyo tu alikuwa mwanachama hodari wa chama chetu, lakini pia katika kipindi chake cha uwakilishi amefanya kazi nzuri na ya kukumbukwa ya kutetea ipasavyo maslahi ya wananchi wa jimbo lake kwa uadilifu na moyo mkubwa wa kujituma,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:
Kupitia kwako Mheshimiwa Spika wa Baraza la Wawakilishi, natuma salamu za dhati ya moyo wangu kwa Wawakilishi wote kwa kuondokewa na wenzao, kwa wananchi wa Bububu kwa kumpoteza mwakilishi wao hodari na kwa wana-CCM wa jimbo hilo kwa kifo cha mwanachama mwenzetu.”
Ameongeza Rais Kikwete: “Aidha, naomba uniwasilishie salamu zangu kwa wanafamilia wote wa Mheshimiwa Mtondoo kwa kupotelewa na mhimili mkuu wa familia. Wajulishe kuwa niko nao katika msiba huu mkubwa. Aidha, nawaombea kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, awape subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo. Naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu. Amen.”
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
17 Machi, 2012 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI