WWANAFUNZI WANANE WAFARIKI DUNIA



WANAFUNZI wanane wa shule ya msingi,Pipaya iliyopo wilayani Ngorongoro Mkoani Arusha, wamefariki dunia baada ya kusombwa na maji wakati wakijaribu kuvuka mto wakati wakitokea shuleni wakielekea nyumbani kwao.
Akidhibitisha kutokea kwa maafa hayo jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Thobias Andengenye alisema kuwa tukio hilo lilitokea tarehe 27 mwezi huu majira ya saa 11.30 jioni katika kijiji cha Kiyaya Wilayani Ngorongoro,mkoani Arusha.
Kamanda aliwataja marehemu hao kuwa ni Olonana Mosirori(13)mwanafunzi wa darasa la saba,Nemao Faraji (14)mwanafunzi wa darasa la tano,Lekinyani Eliakimu(11)mwanafunzi wa darasa la pili,Kisiyaya Mbalinoto(13)mwanafunzi wa darasa la sita na Lapaine Lengukuwi(14)mwanafunzi wa darasa la tano ambao miili yao ilipatikana.
Alisema kuwa tukio hilo lilitokea kufuatia mvua kubwa iliyonyesha jana majira ya saa 9 alasiri wilayani humo na kusababisha maji kujaa katika mito mbalimbali ,kiasi cha wakazi wakiwemo wanafunzi hao kushindwa kuvuka.
Andengenye aliwataja wengine ambao miili yao bado haijapatikana kuwa ni Ponyangusi Mbalau(12)mwanafunzi wa darasa la tano,Logoi Oleiki(11)mwanafunzi wa darasa la pili.
Hata hivyo jeshi la Polisi Wilayani humo kwa kushirikiana na Wananchi wanaendelea kutafuta miili mingine mitatu ambayo bado haijulikani ilipo huku miili ya marehemu iliyopotikana ikikabidhiwa kwa ndugu na jamaa kwaajili ya shughuli za mazishi.
Wakati huo huo Askari wa jeshi la wananchi Tanzania(JWTZ), kikosi cha 977 Tanganyika Packers, Joseph Simsokwe (37)amekutwa amekufa pembezoni mwa korongo ,baada ya kusomwa na maji ya mvua katika eneo la Njiro kwa msola,nje kidogo ya jiji la Arusha.
Kamanda Andengenye alisema kuwa tukio hilo la kukutwa kwa mwili hulo,lilitokea juzi majira ya saa 3 asubuhi ambapo polisi waliokuwa doria waliukuta mwili huo ukiwa umekwama kwenye korongo.
Alisema kuwa mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia askari polisi walifika na walipouchunguza mwili huo walibaini kuwa marehemu alikuwa ni askari wa JWTZ na alikutwa na jeraha kubwa la mshono katika mguu wake wa kulia linalodaiwa kutokana na ajali ya pikipiki.
Kwa mujibu wa majirani na marehemu huyo wamedai ya kuwa mwanajeshi huyo alikuwa akitumia pombe nyingi kupita kiasi na kwamba siku ya tukio anadaiwa kuwa tayari alikuwa amekunywa pombe hali iliyosababisha ashindwe kumudu kuvuka mto na kusombwa na maji yaliyosababisha kifo chake.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospital ya mkoa Mount Meru,kwa ajili ya uchunguzi zaidi ,polisi bado wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo.
Katika tukio jingine,mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Arusha day,mkazi wa Olmatejoo,Emanuel Agrey(15)amejinyonga kwa kutumia kitenge cha mama yake mzazi hadi kufa kwenye kamba ya kuanikia nguo.
Kamanda Andengenye alifafanua kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa 10 jioni katika eneo la Olmatejoo ,ambapo mama mazazi wa marehemu huyo,Magreth Stewart (37) aliukuta mwili wa mtoto wake ukiwa umening’inia kwenye kamba hiyo ya kuwanikia nguo alipokuwa akitoka kanisani.
Alisema kuwa mama huyo baada ya kuona mwili huo alitoa taarifa kwa watu mbalimbali akiwemo mume wake,Agrey Stewart ambapo kwa pamoja waliingia ndani na kushuhudia tukio hilo na baadae walitooa taarifa kituo cha polisi ,ambao askari polisi walifika na kuondoka na mwili huo.
Kwa mujibu wa kamanda Andengenye chanzo cha tukio hilo bado hakijajulikana na kwamba polisi wanachunguza tukio hilo huku na mwili wa mwanafunzi huyo ukiwa umehifadhiwa katika chumba cha maiti katika hospitali ya mkoa mount Meru.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.