Jukwaa la Mabunge ya nchi za SADC kuunda Bunge lake

Na Prosper Minja-Bunge
 
 Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne S. Makinda (Mb) yuko Maputo Msumbiji kuhudhudhuria mkutano wa 31 wa Jukwaa la Mabunge ya nchi wananchama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusinin mwa Afrika- SADC-PF. Mkutano huo ulionza leo tarehe 11 Julai 2012 utajadili pamoja na mambo mengine uwezekano wa kuunda Bunge la SADC. Jambo lingine linalojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja na kuimarisha demokrasia katika chaguzi mbalimbali za nchi wanachama.
Tayari chombo hiki (SADC-PF) kimeanzisha utaratibu wa kusimamia chaguzi mablimbali na kutoa taarifa iwapo katika chaguzi hizo kumekuwa na ukiukwaji wa sheria na taratibu za uchaguzi.
Katika mkutano huo Tanzania imepwa jukumu la kujifunza muundo na uendeshaji wa Bunge la Afrika Mashariki. Wakati huo huo Afrika Kusini imepwa jukumu la kujifunza muundo na utendaji wa Bunge la Umoja wa Ulaya. Nchi hizi mbili zitawasilisha taarifa kwenye kikao cha SADC-PF kitakachofuata ili kuona ni kwa jinsi gani Bunge hilo litakavyoweza kuundwa.
SADC-PF imekuwa mstari wa mbele kutoa misaada na kuelimisha umma kuhusu virusi na kuishi na virusi vya UKIMWI na kujikinga na maambukizi mapya UKIMWI. Aidha chombo hiki kimeshatoa mwongozo wa kisheria kuhusu UKIMWI na jinsi ya kuuhamasisha umma.
Katika Mkutano huo Spika Makinda naongoza ujumbe wa wajumbe watano ambao ni: Mhe. Stella Manyanya, Mhe. Anna Abdallah, Mhe. Habib Mnyaa, Mhe. Titus Kamani na Kaimu Katibu wa Bunge Bwana Jossey Mwakasyuka.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.