Waliobomolewa Mbezi Beach kwenda Mahakamani Wadai wanamiliki maeneo yao kihalali na wameonewa

Na Joachim Mushi wa Thehabari.com
WAKAZI 32 wa eneo la Mbezi Beach Kata ya Kilongawima wanakwenda mahakamani kupinga kitendo cha Serikali kuwabomolea nyumba zao hivi karibuni, kitendo ambacho wanadai wameonewa kwani wao wanamiliki maeneo hayo kihalali, huku baadhi yao wakiwa na nyaraka muhimu za umiliki na baraka kutoka Serikali za Mtaa husika.
Wakizungumza na vyombo vya habari leo wakazi hao wamesema wanasikitishwa na kitendo hicho cha mabavu kufanywa na Serikali tena kwa kuvizia ilhali kulikuwa na taratibu za kisheria za kufuatwa kabla ya zoezi hilo kama kulikuwa na haki ya kufanyiwa hivyo.
Akitoa tamko la wakazi wa eneo hilo leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa wakazi hao, Antony Mseke alisema madai ambayo Serikali kupitia Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) imeyatoa kuwa wao wamevamia eneo la mikoko na kujenga maeneo yasioruhusiwa hayana msingi wowote kwani eneo hilo lipo mbali na mikoko hiyo.
Alisema wanakwenda mahakamani kutafuta haki yao kwa kuwa kilichofanyika ni uvunjaji wa sheria na huenda kuna sababu nyingine wanazo na si kama ilivyotamkwa na waliobomoa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.