WAZAMIAJI sita kutoka Afrika Kusini na Israel, wametua Zanzibar kusaidia shughuli za uopoaji wa watu walikufa na walionusurika katika ajali ya meli ya Mv Skagit, iliyotokea karibu na Kisiwa na Chumbe, Bahari ya Hindi.
Waogeleasji hao wa kujitolea wenye uwezo kuzama hadi kina cha mita 50 tayari wameanza kazi.
Baadhi ya meli zilizositisha kazi ya uokoaji kwa kukosa mafuta, tayari zimeanza kufanya kazi leo asubuhi baada ya kupata nishati hiyo.
Meli hiyo imezama kufikia kina cha mita 28 chini ya Bahari ya Hindi.
Kuhusu taarifa kamili kuhusu meli hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uasafiri wa Zanzibar, Abdallah Kombo amesema zipo SUMATRA Tanzania Bara. Idadi kamili ya abria waliopanda meli hiyo bado ni kitendawili.
Waogeleasji hao wa kujitolea wenye uwezo kuzama hadi kina cha mita 50 tayari wameanza kazi.
Baadhi ya meli zilizositisha kazi ya uokoaji kwa kukosa mafuta, tayari zimeanza kufanya kazi leo asubuhi baada ya kupata nishati hiyo.
Meli hiyo imezama kufikia kina cha mita 28 chini ya Bahari ya Hindi.
Kuhusu taarifa kamili kuhusu meli hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uasafiri wa Zanzibar, Abdallah Kombo amesema zipo SUMATRA Tanzania Bara. Idadi kamili ya abria waliopanda meli hiyo bado ni kitendawili.
Comments