Mbio mpya za Magari ya Umeme
Katika ulimwengu wa mbio za magari injini inayotegemea joto ndiyo mtawala.
Chama kinachotawala mchezo wa magari FIA, kimetangaza mipango mipya ya mbio za magari iliyobuniwa kwa magari yanayotumiwa nguvu ya umeme pekee.
Mashindano mapya , yatakayojulikana kama Formula E, yanatazamiwa mwaka 2014.
Makampuni yanayotengeneza magari yameombwa kaunde magari yao yenyewe , ambayo yatashiriki mbio za mitaa ya mijini kote Duniani.
Mashindano haya yataendeshwa na shirika la Formula E Holdings, ushirika wa wawekezaji kadhaa wakiongozwa na tajiri mmoja wa Uhispania Enrique Banuelos, aliyetengeneza ma-bilioni ya dola zake kupitia biashara ya ujenzi wa nyumba na kilimo.
Shirika la FIA linasema kua mpango huo ni kuangazia majaliwa ya magari ya baadaye kwa miongo mingi ijayo.
Comments