Mbio mpya za Magari ya Umeme


Magari ya mbio Formula 1

Katika ulimwengu wa mbio za magari injini inayotegemea joto ndiyo mtawala.

Viwanja vya mduara kwa mashindano ya magari ya Langalanga daima husikika miliyo inayopausa masikio kwa uwezo wa injini zenye nguvu kubwa kama V10 na V12. Ingawa utawala wa injini hizo zinazotegemea joto unakaribia kwisha.

Chama kinachotawala mchezo wa magari FIA, kimetangaza mipango mipya ya mbio za magari iliyobuniwa kwa magari yanayotumiwa nguvu ya umeme pekee.

Mashindano mapya , yatakayojulikana kama Formula E, yanatazamiwa mwaka 2014. 

Makampuni yanayotengeneza magari yameombwa kaunde magari yao yenyewe , ambayo yatashiriki mbio za mitaa ya mijini kote Duniani.

Mashindano haya yataendeshwa na shirika la Formula E Holdings, ushirika wa wawekezaji kadhaa wakiongozwa na tajiri mmoja wa Uhispania Enrique Banuelos, aliyetengeneza ma-bilioni ya dola zake kupitia biashara ya ujenzi wa nyumba na kilimo.

Shirika la FIA linasema kua mpango huo ni kuangazia majaliwa ya magari ya baadaye kwa miongo mingi ijayo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI