NMB YANG’ARA KATIKA MAONYESHO YA NANE NANE 2012
Nanena Dodoma
Banda la NMB Arusha
Banda la NMB Morogoro
Na Mwandisi Wetu
Kilimo ndiyo shughuli kuuyauchumi Tanzania. NMB ikiwa benki yenye mtandao mpana zaidi Tanzania inatambua umuhimu wa kilimo kwa maendeleo ya Tanzania. Ili kuchochea maendeleo ya kilimo, NMB ilikuwa benki ya kwanza kuanzisha akaunti maalum kwa ajili ya wakulima iitwayo NMB Kilimo Account.
Pia NMB imeanzisha huduma ya mikopo kwa ajili ya mazao mengi ya kilimo ikiwemo chai, kahawa, miwa, alizeti, korosho na mazao mengine.
Ili kuelimisha umma juu ya huduma mbalimbali za kilimo NMB inashiriki kwenye maonyesho ya NaneNane Morogoro, Dodoma, Arusha, Mbeya, Lindi na Songea, Tabora na Shinyanga.
Akizungumza juu ya ushiriki wa NMB kwenye NaneNane Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NMB, Imani Kajula amesema, “NMB inatambua umuhimu wa kilimo kwa maendeleo ya Tanzania ndiyo maana NMB imekuwa mstari wa mbele kubuni bidhaa na huduma maalum za sekta ya kilimo.
Mbali na ushiriki NMB ni moja ya wadhamini wa maonyesho ya kitaifa yanayofanyika Dodoma”.
Comments