AFARIKI AKIVUA SAMAKI


Na Ezekiel Kamanga,Chunya.
Mwananchi mmoja aliyefahamika kwa jina la Emmanuel Kidava,amefariki dunia akivua samaki katika Kitongoji cha Kambipotea,Kijiji cha Iyovyo,Kata ya Totowe Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya.

Tukio hilo limetokea Septemba 19 mwaka huu majira ya saa 2 asubuhi,marehemu akiwa na Mtumbwi alipokwenda kuvua samaki na mauti hayo yamemkuta alipokuwa akivuta nyavu alizotega samaki,lakini nyavu hizo zilikwama kwenye mwamba ndipo marehemu alichupa kupiga mbizi ndani ya maji ili kujaribu kuzinasua nyavu hizo.

Aidha katika juhudi hizo za kunasua nyavu hizo marehemu alikosa hewa na dakika tatu baadae alipoteza maisha kutokana na kunasa katika nyavu hizo alizokuwa akijaribu kuzinasua.

Baada ya kushindwa kuibuka baadhi ya wavuvi waliokuwa karibu baada ya kuona marehemu haibuki baada ya kuzama walifuatilia eneo la tukio na kuanza kuvuta nyavu hizo hadi ufukweni mwa ziwa na kumkuta marehemu kapoteza maisha.

Wavuvi hao baada ya kuutoa mwili wa marehemu katika maji walitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Kambipotea Bwana Richard Mbuya,ambapo alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na yeye kuitaarifu Polisi.

Jeshi la Polisi lilifika eneo la tukio na kuruhusu mwili huo kuchukuliwa kwa ajili ya maziko,kutokana na marehemu kutokuwa na ndugu hivyo Serikali ya kijiji ilichukua jukumu la mzishi,

Hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa marehemu kabla ya kifo chake imedaiwa alitokea katika Kijiji cha Nzihi,barabara ya kuelekea Kidamali Mkoani Iringa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.