CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI DODOMA CHALAANI MAUAJI YA MWANDISHI DAUD MWANGOSI

SEPTEMBER 03.2012 MAUAJI……
CHAMA cha waandishi wa habari mkoa wa Dodoma (CPC)wamelaani vurugu
zilizotokea juzi mkoani Iringa na kusababisha kifo cha mwandishi wa
habari wa kituo cha utangazaji cha Chanel Ten Daud Mwangosi.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa chama hicho Habel Chidawali
alipokuwa akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari mkoani hapa.
Chidawali amesema kuwa kamwe chama hicho hakikubaliani na nguvu kubwa
iliyotumiwa na jeshi la polisi kwa ajili ya kumwaga damu ya mwandishi
huyo ambaye hakuwa na hatia na kamwe jeshi la polisi haliwezi
kujitetea kwa kudai kifo cha mwandishi huyo ni bahati mbaya.

Amesema kuwa
 jeshi la polisi limekuwa likionyesha wazi wazi kuwa
linatumia nguvu,ubabe na matumizi mabovu ya silaha za moto ambayo
hayajaweza kusaidia siku zote na badala yake kinachoachwa ni maumivu
na vilio kwa wananchi.

Katibu huyo amesema kama jeshi la polisi linatuliza ghasia hakuna
siku hata moja haijatokea wakamuua kiongozi yoyote wa siasa ambao ni
vinara wa mikutano mbalimbali.

Kwa upande wao wananchi mbalimbali mkoani hapa wamekemea nguvu kubwa
inayotumika na Polisi katika vurugu mbalimbali zinazotokea.
Wamesema tabia ya jeshi la polisi kutumia nguvu na silaha za moto
ambazo zinasababisha vifo vya watu wasiokuwa na hatia.

Catheline Muhinte, amesema kuwa tukio lililofanywa na jeshi la polisi
la kumuua mwandishi wa habari linaonyesha dhairi kuwa kwa sasa jeshi
hilo linafanya kazi kwa kukiuka maadili ya malengo yao.

Amesema katika mwonekano wa picha ambazo zinaonekana katika vyombo
mbalimbali vya habari
 inaonyesha dhairi kuwa polisi walihusika moja
kwa moja na kifo cha mwandishi huyo.
M/Masasi from Tanzania Regions Blogs Reporting…………….

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI