Chipolopolo yailipua Cranes

Mabingwa wa Afrika Zambia wamewafunga Uganda bao 1-0 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Levy Mwanawasa , mjini Ndola ,zambia, Jumamosi.

Hii ilikuwa mechi ya kuwania kufuzu kucheza fainali za kombe la Afrika za mwaka 2013, Afrika kusini.

Nahodha wa Chipolopolo Christopher Katongo alifunga goli kutokea katikati ya uwanja kipindi cha kwanza cha mchezo.

Mchezaji huyo anayesakata soka ya kulipwa nchini China alitumia mwanya wa kuzubaa kwa mabeki wa The Cranes kunasa mpira wa kurusha wa Davies Nkausu na kufurahisha mashabiki wapatao 40,000 waliohudhuria mechi hiyo.

Uganda, inasaka nafasi kwa mara ya kwanza kucheza fainali za kombe la Afrika (AFCON) tangu mwaka 1978 ilipomaliza mshindi wa pili nyuma ya wenyeji Ghana.

Timu hizo mbili zitarudiana nchini Uganda katikati ya mwezi Oktoba, mwaka huu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.