Dk. Mwinyi afanya ziara NHIF

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Emanuel Humba akiongozana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi na wajumbe wa Bodi kukagua miradi ya Mfuko huo.

Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emanuel Humba akitoa maelezo ya moja ya miradi ya Mfuko huo kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussen Mwinyi.

Mkurugenzi wa Uwekezaji na Fedha, Deusdedit Rutazaa akitoa maelezo ya Mradi kwa Waziri na viongozi wengine wa Mfuko.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi akitoa maelekezo kwa viongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuhusiana na miradi iliyowekezwa Makao Makuu ya Mfuko huo.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Ally Kiwenge akitoa salaam za Bodi kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii akizungumza na wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya alipofanya ziara makao makuu ya Mfuko huo leo.

Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (walioko mbele) wakisikiliza kwa makini maelekezo ya Waziri wakati akizungumza na wafanyakazi.

Wafanyakazi wakisikiliza kwa makini maelekezo ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.

Wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wakimsikiliza Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii alipofika kwa lengo la kuzungumza nao.
Kuna haja ya kuwa na mdhibiti huduma za afya-Dk. Mwinyi

SERIKALI imesema kuna haja ya kuwepo kwa chombo maalum cha kudhibiti mfumko wa bei katika sekta ya afya kwa lengo la kuwawezesha wananchi wake kupata huduma hizo bila kuwepo kwa vikwazo vya gharama kubwa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi wakati akizungumza na wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) alipotembelea Makao Makuu ya Mfuko huo.

Hatua ya Dk. Mwinyi kusema hayo ilitokana na ombi la Wafanyakazi hao kupitia Mwenyekiti wa Tawi la Chama cha Wafanyakazi (TUGHE), Baraka Maduhu, ambaye alisema kati ya mambo yanayowanyima faraja wafanyakazi wa Mfuko huo ni pamoja na mfumko holela wa gharama za matibabu.

“Pamoja na mafanikio makubwa ambayo Mfuko umeyafikia lakini bado kuna vikwazo ambavyo sisi kama wafanyakazi wa Mfuko vinatunyima faraja likiwemo la upandishwaji holela wa gharama za matibabu hatua itakayowafanya Watanzania na Mfuko kwa ujumla kushindwa kumudu gharama hizo hivyo ombi hili tunalileta kwako,” alisema Mwenyekiti wa TUGHE.

Akijibu hoja mbalimbali ambazo ziliwasilishwa kwake kama kero za wafanyakazi wa Mfuko, Dk. Mwinyi alikubaliana na ombi hilo na kusema kuna haja kubwa ya kuwepo kwa chombo hicho ili kiweze kulinda walaji kwa kuwa suala la kupata huduma za matibabu kwa mwananchi ni suala nyeti linalogusa maisha ya mwananchi moja kwa moja.

Kutokana na hali hiyo, Waziri alisema kinachotakiwa kufanyika kwa sasa ni kupata maoni ya wadau mbalimbali wa sekta ya afya ili kuangalia namna ya utekelezaji wake.

Katika hatua nyingine Dk. Mwinyi aliupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuwa ni moja ya Taasisi ambayo iko chini ya Wizara yake inayofanya vizuri katika utekelezaji wa shughuli zake.

“Mkifanya vizuri tunapaswa kuwaambia na mnapokosea ni lazima tuwaonye lakini ninachoweza kusema kwa sasa ni kwamba uongozi na wafanyakazi kwa ujumla mnafanya vizuri hivyo ongezeni bidii ili kufikia malengo mliyoyaweka nay a Serikali kwa ujumla,” alisema.

Akizungumzia suala kuwepo kwa chombo maalum chini ya wizara kitakachodhibiti ubora wa huduma zinazotolewa na Bima za afya zikiwemo za binafsi na serikali kama zinakidhi kiwango cha ubora wa huduma ikilinganishwa na michango ya wanachama, Dk. Mwinyi alikubaliana na wazo hilo na kusema kuna haja ya suala hilo kuwa chini ya wizara ili liweze kuwa na usimamizi mzuri.

“Pamoja na suala hili kuwa chini ya Wizara ya Fedha ambayo inaangalia bima kwa ujumla wake lakini masuala ya afya ni masuala nyeti na yanayotakiwa kuangaliwa kipekee hivyo kuna haja ya kuwa na chombo kinachosimamia bima za afya,” alisema.

Akitoa maelezo ya utangulizi, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Emanuel Humba, alisema kitendo cha Waziri kutembelea na kuzungumza na wafanyakazi kinaleta faraja kwa wafanyakazi lakini pia kuongeza juhudi ya utendaji zaidi hivyo akamwomba Waziri kutochoka kufanya hivyo mara kwa mara.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.