Jeshi la Kenya lakiri mauaji ya wasomali 6


Jeshi la Kenya limekiri kuwa mwanajeshi wake mmoja alifyatua risasi na kuwaua raia sita wa somalia mnamo siku ya Jumapili.
Jeshi la Kenya lenyewe limesema kuwa linafanya uchunguzi na kwamba litachukua hatua zinazostahili.
Uftyauaji risasi ulitokea katika kijiji cha Jana Abdalla, ambacho kiko umbali wa kilomita sita kutoka mji wa Kismayo ambao umekuwa ngome kubwa ya wapiganaji wa Al Shabaab.
Msemaji wa jeshi la Kenya Kanali Cyrus Oguna alikana madai kuwa mauaji hayo yalifanywa kwa maksudi na kuelezea kuwa wanajeshi wake walivamiwa na wanamgambo hao ambao waliwaua wanajeshi wawili wa Kenya.
Hapo awali Ujumbe wa Umoja wa Afrika wa kudumisha amani nchini Somalia AMISOM, ulisema utachunguza mauaji hayo.
Msemaji wa kikosi cha Somalia, Mohemmed Hirsi, ameiambia BBC kuwa mauaji hayo yalitokea wakati jeshi la Kenya lilipovamiwa na wapiganaji wa Al Shabaab takriban kilomita sitini kutoka kwa ngome kubwa ya kundi hilo.
Msemaji wa AMISOM kanali Adi Aden amesema wakati ukweli wa kesi hiyo utakapojulikana watachukua hatua.
Msemaji huyo aliambia BBC kuwa wanajeshi wa Kenya waliwafyatulia risasi wanaume hao waliokuwa wameketi nje ya duka moja katika kijiji cha Janaay Cabdalla.
Wanajeshi wa Kenya na wale wa Somalia awali walivamiwa na wapiganaji wa Al Shebaab huku ripoti zikisema kuwa pande hizo mbili, zilipata majeruhi.
Kwa mujibu wa msemaji huyo, wanakijiji waliouawa ambao ni wanaume saba hawakuwa wanamgambo bali raia wa kawaida.
Duru zinasema kuwa wanaume hao walikuwa wamepiga foleni kununua sukari.Aidha msemaji wa jeshi la Muungano wa Afrika nchini Somalia, (AMISOM) alisema kuwa hawezi kuthibitisha tukio hilo, lakini madai hayo yatachunguzwa.
Wanajeshi wa Somalia wakiungwa mkono na wale wa Uganda na Kenya pamoja na vikosi vingine kutoka nchi tofauti za Afrika, wanakaribia kuuzingira mji wa Kismayo,na ili waweze kufanikiwa katika kuuteka mjihuo, wanachi wa pale watahitaji kushirikiana nao.
Wanajeshi wa Kenya wamewahi kutuhumiwa kwa kuwaua raia wakati wakifanya mashambulizi katika maeneo ya Al Shabaab .
Shirika la kuwahudumia wakimbizi UNHCR linakadiria takriban wakimbizi 10,000 wameutoroka mji wa Kismayo katika kipindi cha wiki moja iliyopita.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI