MWALUSAKO, CHAMBUA, SHEMEJI YAKE KIKWETE WAULA YANGA
Mwalusako |
Na Mahmoud
Zubeiry
BEKI wa
zamani wa Yanga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Lawrence Mwalusako
atakaimu nafasi ya Katibu wa klabu hiyo, kufuatia kusimamishwa kwa Celestine
Mwesigwa, wakati kiungo wa zamani wa klabu hiyo, Sekilojo Johnson Chambua
atakuwa Meneja mpya wa klabu hiyo, akirithi mikoba ya Hafidh
Saleh.
Habari
kutoka ndani ya Yanga, zimesema kwamba viongozi hao wapya watatangazwa wakati
wowote kuanzia sasa kurithi nafasi za viongozi walioondolewa madarakani,
kutokana na kile kilichoelezwa utendaji
usioridhisha.
Nafasi
nyingine za Mhasibu mpya, iliyoachwa wazi na Philip Chifuka itakuwa chini ya
dada mmoja, aliyetajwa kwa jina moja tu, Rose aliyekuwa akifanya kazi ofisi hiyo
kwa muda mrefu, wakati Msemaji wa klabu iliyoachwa wazi na Louis Sendeu,
inaelezwa atapewa mdogo wa mke wa Ridhiwani Kikwete, aliyehesabu kura za
Abdallah Bin Kleb katika uchaguzi mdogo wa klabu, Julai 14.
Mapema leo
mchana, uongozi wa Yanga ya Dar es Salaam, umeisimamisha kazi Sekretarieti nzima
ya klabu, akiwemo Katibu Celestine Mwesigwa na Ofisa Habari, Louis Sendeu,
kutokana na kile ilichoeleza utendaji
usioridhisha.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari, makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam, Makamu
Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga alisema kwamba maamuzi hayo yamefuatia kikao
cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika tangu saa 5:30 leo hadi saa
9:30.
Wengine
wanaokumbwa na panga hilo ni Masoud Saad, aliyekuwa Ofisa Utawala, Philip
Chifuka aliyekuwa Mhasibu na Hafidh Saleh aliyekuwa Meneja ambaye anahamishiwa
kwenye majukumu mengine.
“Tumesitisha
mikataba ya sekretarieti nzima, pia tumefanya marekebisho, tumemtoa Meneja wa
timu na muda si mrefu tutamtangaza Meneja mwingie pamoja na sekretarieti
mpya,”alisema Sanga.
Aidha, Sanga
alisema Kocha Mbelgiji, Tom Saintfieti anapewa onyo kali kwa kuzungumza ovyo na
vyombo vya habari.
“Tumekwishakutana
naye mara kadhaa kumpa utaratibu wa kuzungumza na vyombo vya habari, sasa
tutamuandikia barua ya kumkumbusha wajibu wake na kuzingatia wajibu wake,
kutozungumza na vyombo vya habari
holela,”alisema.
Kwa ujumla
maamuzi haya yanakuja baada ya Yanga kuanza vibaya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara, ikiambulia pointi moja tu katika mechi zake mbili za awali, kutokana na
sare ya bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya Jumamosi
na Jumatano ikachapwa mabao 3-0 Morogoro Uwanja wa Jamhuri,
Morogoro.
Mwalusako
amewahi kuwa Katibu wa Yanga, wakati wa Wakili Imani Madega Mwenyekiti wa klabu
hiyo na akalazimika kujiuzulu kwa tuhuma mbalimbali zinazohusu uwajibikaji na
uadilifu kwa kwa ujumla, wakati Chambua amewahi pia kuwa Meneja wa Yanga kwa
muda na akakumbwa na mabadiliko ya kawaida.Kwa hisani ya Bin Zubeiry Blog
Comments