Jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe lililopo Kisarawe
mjini Mkoani Pwani. Jengo hili ni la kisasa ambalo lina korti mbili,
mahabusu ya wanawake na ya wanaume, vyoo vya ndani na nje, stoo na ofisi
mbalimbali
Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Angellah Jasmine Kairuki akipata
maelezo kutoka kwa Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Mh. Jaji Mmila
alipofanya ziara ya kikazi jana (20/09/2012) ya kutembelea baadhi ya
Mahakama nchini ikiwemo Mahakama Kuu ya Tanzania, Mahakama ya Mwanzo
Kimanzichana, Mahakama ya Wilaya Kisarawe na Mahakama ya Mwanzo Kibaha
Maili Moja.
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Wilaya ya Mkuranga Mh.
Abdala A. Pendekezi (wa pili kulia) akimwonesha kiwanja kitakachojengwa
Mahakama ya Mwanzo Kimanzichana Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mh.
Angellah Jasmine Kairuki (wa kwanza kulia) alipofanya Ziara ya Siku moja
ya kutembelea Mahakama nchini. Wa kwanza Kushoto waliosimama mbele ni
Naibu MKurugenzi wa Mahakama za Mwanzo Mh. Warsha Numbu, anayefuatia nI
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mh. Mercy Sila
Comments