GS
Taarifa kwa
Vyombo vya Habari
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu
Tanzania limeteua wadau 10 kwa ajili ya kusaidia timu ya taifa ya vijana walio
na umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys itakayopambana na Congo (Brazaville)
katika mechi ya raundi ya tatu ya michuano ya awali ya Mataifa ya
Afrika.
Uteuzi huo umefanywa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga baada ya Kamati
ya Vijana ya TFF kufanya kikao chake kujadili kwa umakini ushiriki wa timu hiyo
na kupeleka mapendekezo yake kwa rais huyo wa shirikisho.
Kutokana na umuhimu wa mechi hiyo itakayoamua timu itakayofuzu
kucheza fainali za Mataifa ya Afrika, TFF imeona umuhimu wa kuwa na kamati
ambayo itakuwa na majukumu mawili makubwa ambayo ni:
1.
Kuhamasisha vijana waone umuhimu
na kuwa na ari ya kushinda mechi hiyo
2.
Kuhamasisha umma uone umuhimu wa
mechi hiyo na hivyo kuisaidia iweze kufuzu.
Walioteuliwa kuunda kamati hiyo ni:
1.
Ridhiwani
Kikwete
Mwenyekiti
2.
Ahmed Seif
(Magari) Mjumbe
3.
Nassoro Bin
Slum
Mjumbe
4.
Henry
Tandau
Katibu
5.
Ahmed
Mgoyi
Mjumbe
6.
Aboubakar
Bakhresa Mjumbe
7.
Angetile
Osiah
Mjumbe
8.
Kassim
Dewji
Mjumbe
9.
Abdallah Bin
Kleb
Mjumbe
10.
Salim
Said
Mjumbe
Baada ya kuvuka raundi mbili za kwanza bila ya kucheza mechi
kutokana na wapinzani wake kujitoa, timu ya Serengeti Boys inahitaji kufanya
kila iwezalo kuweza kuiondoa Congo kwenye mashindano hayo na kuweka rekodi ya
kufuzu kucheza fainali hizo za Afrika ambazo pia zitatoa wawakilishi wa Afrika
kwenye mashindano ya Kombe la Dunia. Mechi za kwanza za raundi ya tatu
zitachezwa kati ya Novemba 16 na 18, 2012 na mechi za marudiano zitachezwa
kuanzia Novemba 30, 2012 hadi Desemba 2, 2012
*Kuhusu suala la Azam FC kuwasimamisha wachezaji watatu kwa tuhuma
za kuhusika kuhujumu timu, tayari TFF imepokea barua hiyo ya Novemba 8, 2012 na
inalishughulikia na kulifuatilia kwa makini.
*TFF inapenda kukipongeza Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa
Mwanza kwa kufanya uchaguzi wake kwa amani na kufanikiwa kupata viongozi wapya
watakaokuwa chini ya uenyekiti wa Jackson Songora. Rais wa TFF amewapongeza
viongozi waliorekjea madarakani na viongozi wapya akieleza magtumaini yake kuwa
kamati mpya ya Utendaji ya MRFA itaelekeza nguvu zake katika kuendeleza mikakati
iliyokuwepo ya kuinua kiwango cha mpira wa miguu na kubuni mikakati mingine
kwenye mkoa huo na Tanzania kwa ujumla ikishirikiana na TFF.
*Ligi Kuu ya Vodacom inatazamiwa kuendelea kesho kwenye viwanja
tofauti
1. Simba v Toto
Africans Uwanja wa
Taifa
2. T. Prisons v JKT
Ruvu Sokoine
3. Kagera Sugar v Polisi
Moro Kaitaba
4. African Lyon v Mtibwa
Sugar Azam Complex
5. Oljoro JKT v Ruvu
Shooting Sheikh Amri
Abeid
6. Mgambo JKT v Azam
FC Mkwakwani
Jumapili
1.
Coastal Union v
Young Africans Mkwakwani
Comments