LIGI YA MABINGWA ULAYA: AC MILAN, PSG, SCHALKE 04, ARSENAL, DORTMUND ZAFUZU 16 BORA


 Hii ilikuwa ni mechi kati ya Anderlecht dhidi ya AC Milan, ambapo Milan ilishinda mabao 3-1
 Jack Wilshere wa Arsenal akiifungia timu yake ilipoumana na Montpellier ya Ufaransa. Arsenal ilishinda 2-0
Hili lilikuwa ni pambano baina ya mabingwa wa 'Eredivise' Ajax ya Uholanzi, dhidi ya mabingwa wa 'Bundesliga' Borussia Dortmund ya Ujerumani. Dortmund ilishinda mabao 4-1
MONACO, Ufaransa
Mabingwa wa Bundesliga, Borussia Dortmund wamefuzu 16 bora kutokea kundi D kwa ushindi wa mabao 4-1 ugenini Amsterdam ArenA dhidi ya wenyeji Ajax, huku Real Madrid wakiungana na Wajerumani hao baada ya sare dhidi ya Man City
BEKI Philippe Mexes alifunga bao tamu akiwa amelipa mgopngo lango la maadui kuipa AC Milan tiketi ya kufuzu hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa ushindi wa mabao 3-1 ugenini dhidi ya Anderlecht.
Mfaransa huyo alifunga bao hilo kuongeza lile la ufunguzi la Stephan El Shaarawy, kabla ya Alexandre Pato kupigilia msumari wa mwisho katika jeneza za Wabelgiji hao.
Paris St-Germain imesonga hatua inayofuata kutokea kundi A, huku Schalke na Arsenal wakitinga mtoano wa 16 bora kutokea kundi B.
Mabingwa wa Bundesliga, Borussia Dortmund wamefuzu 16 bora kutokea kundi D kwa ushindi wa mabao 4-1 ugenini Amsterdam ArenA dhidi ya wenyeji Ajax, huku Real Madrid wakiungana na Wajerumani hao baada ya sare dhidi ya Man City.
Katika mechi za kundi A, Ezequiel Lavezzi alikuwa shujaa wa PSG, akifunga bao moja kila kipindi kuipa klabu hiyo ya Ligue 1 ushindi wa 2-0 ugenini dhidi ya Dynamo Kiev. Mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic, alikuwa mpishi mkuu wa Lavezzi katika mechi hiyo.
Kwa ushindi huo, PSG chini ya Carlo Ancelotti kimesimama kwa pointi moja nyuma ya vinara Porto, ambao walishafuzu mtoano wa 16 bora kabla hata ya juzi kuichapa Dinamo Zagreb mabao 3-0. Zagreb sasa inaburuza mkia bila pointi, huku Kiev ikifuzu Europa League.
Katika kundi la B, Christian Fuchs aliifunga bao pekee dakika ya 13 kuipa Schalke 04 tiketi ya kufuzu mtoano kwa ushindi wa 1-0 nyumbani dhidi ya Olympiakos. Ushindi huo umewabakisha kileleni mwa kundi, licha ya Arsenal, kushinda 2-0 dhidi ya Montpellier.
Schalke itaweza kumaliza kinara wa kundi hilo, kama itamudu kuichapa Montpellier katika mtangane wa mwisho makundi, huku Olympiakos tayari ikiwa na tiketi ya kufuzu Europa League kwa kushika nafasi ya tatu ya kundi hilo.
Katika kundi C, licha ya PSG kushinda mabao mabao 3-1 dhidi ya Anderlecht, Malaga ya Hispania imeendelea kubaki kileleni mwa kundi hilo, licha ya kulazimishwa sare ya 2-2 dhidi ya Zenit St Petersburg – ambayop imeambulia kutinga katika Europa League.
Katika mitanange ya Kundi la Kifo la D, Robert Lewandowski aliifungia mara mbili Borussia Dortmund na kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Ajax.
Katika mechi hiyo, Marco Reus alifunga bao la ufunguzi, kisha Mario Goetze kufunga la pili, huku Daniel Hoesen akifunga la kufutia machozi la Ajax.
Real Madrid ilijikuta ikiambulia sare ya bao 1-1 Etihadi yaliko makazi ya Manchester City na kujihakikishia nafasi ya pili ya kundi hilo.
Sare imeing’oa Man City katika michuano hiyo, ingawa inaweza kufuzu Europa League, lakini kama tu itafanikiwa kuichapa Dortmund katika mechi ya mwisho, huku ikiiombea mabaya Ajax itakapoumana na Madrid huko Bernabeu katika mechi za mwisho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI