MABINGWA WA BALIMI BOAT RACE MWANZA WAPATIKANA
Mabingwa wa Mashindano ya Mitumbwi ya Balimi mkoa wa Mwanza, timu
ya Cheka na Wengi kutoka Misungwi, wakiwasili ufukweni baada ya kuongoza mbio
hizo zilizofanyika Mwaloni mkoani humo juzi. (Na Mpiga Picha Wetu)
Daniel Mugeng'a Nahodha wa Timu ilishinda wa naume kutoka Misungwi akionyesha kitita cha kaki tisa baada ya kukabidhiwa
Mabingwa wa mashindano ya Mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race)
Mkoani Mwanza upande wa wanawake timu ya Wanawake na Maendeleo kutoka Misungwi
wakiwa hawaamini kama wameweza kushinda kwa kuwaacha mbali wenzao na kuwa
mabingwa wa mkoa huo na kukabidhiwa jumla ya shilingi laki saba (700,000) kama
zawadi ya ushindi wa kwanza.
Wapiga makasia wakinyosha makasia yao juu kabla ya kuanza kwa fainali
za mashindano ya mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) yaliyofanyika jijini
Mwanza
Mabingwa wa ngoma za asili wa mashindano ya ngoma ya kanda ya ziwa
kikundi cha Bujora wakitumbuiza mashabiki wa mashindano ya mitumbwi
yaliyofanyika kwenye fukwe za Mwaloni Mkoani Mwanza ambapo washindi
watawakilisha mkoa huo kwenye fainali wamepatikana.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL akiteta jambo na
Afisa Utamaduni na Michezo wa Manispaa ya Ilemela wakati wa mashindano ya
Mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) yaliyofanyika Mkoani Mwanza.
Msanii wa kikundi cha ngoma cha Bujora akichezea nyoka kwa kuingiza
kichwa mdomoni wakati wakitumbuiza watu waliofika kushuhudia mashindano ya
mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) yaliyofanyika Mwaloni Mkoani Mwanza
Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL Fimbo Butallah,
akimuelekeza jambo Nahodha wa timu ya Wanawake na Maendeleo ya Misungwi, Tabu
Daudi, ambao ndio washindi wa kwanza kwa upande wa wanawake Mkoa wa Mwanza mara
baada ya kukabidhiwa zawadi yao ya ushindi wa kwanza kitita cha shilingi laki
saba (700,000).
Comments