MUUMINI AITOSA TWANGA PEPETA AIBUKIA VICTORIA SOUND
Na Asha Bani
Aahidi kufanya kila analoweza kuipandisha chati bendi hiyo na kutamba kama nyingine
huku akikiri kuwa na changamoto kubwa kuondoka Twanga na kuhamia bendi
ndogo ya Victoria, jambo linalomfanya ajiumize ili kulilinda jina lake.
MWANAMUZIKI
nyota wa dansi Tanzania,
Mwinjuma Muumini, ametangaza rasmi kuondoka Twanga Pepeta na kujiunga na bendi
ya Victoria Sound ya jijini Dar es
Salaam.
Muumini
aliyepata kuwika na bendi mbalimbali hapa nchini zikiwamo Mchinga Sound na
Double M, alisema jijini Dar es Salaam jana
kwamba, ameingia mkataba wa miaka miwili na Victoria Sound.
Aliongeza,
atafanya kila analoweza kuipandisha chati bendi hiyo na kutamba kama nyingine huku akikiri kuwa na changamoto kubwa
kuondoka Twanga na kuhamia bendi ndogo ya Victoria, jambo linalomfanya ajiumize
ili kulilinda jina lake.
Comments