SERENGETI YAWAPA RAHA WATANZANIA

Mfungaji wa bao la Serengeti, Mudathir Yahya Abbas kushoto akishangilia huku akipongezwa na wenzake Joseph Kimwaga Lubasha na Ismail Adam Gambo. 

Kwa hisani ya Bongo Staz Blog
TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys leo imeifunga  1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu na ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza Fainali za vijana wa umri huo Afrika zitakazopigwa nchini Morocco mwakani.
Kwa matokeo hayo, Serengeti sasa inahitaji hata sare yoyote katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo mjini Brazzaville ili kukata tiketi ya Morocco mwakani.
Kwa ujumla Serengeti walipigana katika mchezo wa leo, kwani wapinzani wao walionekana kuwa bora na wenye uzoefu zaidi yao.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Miiro Nsubuga, aliyesaidiwa na Mark Ssongo, Balikowa Ngobi na Ronnie Kalemba wote kutoka Uganda, hadi mapumziko Serengeti walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililopatikana dakika ya 15.
Bao hilo lilifungwa kwa shuti la mpira wa adhabu na beki Mudathir Yahya Abbas kutoka umbali wa mita 22 na mpira kabla ya kutinga nyavuni ulimbabatiza beki mmoja wa Kongo na kumpoteza njia kipa Ombandza Mpea Joe na kujaa nyavuni.
Faulo hiyo ilitokana na kiungo wa Serengeti, Hussein Twaha Ibrahim ‘Messi’kuangushwa na beki Okombi Francis wakati akiwa analekea kwenye eneo la hatari la Wakongo.
Baada ya bao hilo, Wakongo walijaribu kuongeza jitihada kiuchezaji, lakini ukuta imara wa Serengeti ulioongozwa na kipa Peter Manyika uliwazuia kusawazisha hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinatimia.
Baada ya mechi hiyo, kocha wa Serengeti Boys, Mdenmark, Jacob Michelsen aliwapongeza vijana wake, lakini akasema bado wana kazi kubwa mbele yao.
Kocha wa Kongo, Mfaransa Eddie Hudanski alitolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 88, baada ya awali kuonywa kwa kutoa lugha chafu, lakini akarudia.
Refa Nsubuga alitoa kadi moja tu ya njano kwa Issambey Lonvreve aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ibara Vinny.
Tanzania; Peter Manyika Peter, Miza Kriston Abdallah, Mohamed Hussein Mohamed, Ismail Adam Gambo, Miraj Adam Suleiman, Mudathir Yahya Abbas, Mohamed Salum Haroub, Joseph Kimwaga Lubasha/Dickson Isaac Ambundo, Hussein Twaha Ibrahim, Suleiman Hamisi Bofu/Tumaini Baraka Mosha na Farid Mussa Shah.
Kongo Brazzaville; Ombandza Mpea Joe, Tmouele Ngampio, Mabiala Gharlevy, Okimbi Francis, Ondongo Boungena, Ibra Vinny/Issambey Lonvreve, Binguila Handy, Obassi Ngatsongo, Mohendiki Brel, Atoni Mavoungou na Biassadila Arei.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.