WAZIRI NCHIMBI KUZINDUA NAMBA MPYA ZA MAGARI YA MAGEREZA
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI, EMMANUEL NCHIMBI
DAR ES SALAAM, Tanzania
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel
Nchimbi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi uzinduzi wa namba mpya za magari ya Jeshi
la Magereza. kesho kutwa Novemba 24.
Kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa kwenye vyombo
vya habari na kusainiwa na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza (CP),
Chamulesile, ilieleza kuwa uzinduzi huo utafanyika kuanzia saa 4:00 asubuhi
katika Gereza Kuu la Ukonga jijini Dar es Salaam.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa uzinduzi huo unazingatia
Sheria ya Usalama Barabarani Sura ya 162 iliyofanyiwa marekebisho ya kanuni ya
Usalama Barabarani (Amendment, ya 2004).
Taarifa hiyo ilisema kuwa, marekebisho hayo yalitangazwa kwenye Gazeti
la Serikali Na.102 la Machi 23 mwaka huu, na yalitoa nguvu ya kisheria kwa
magari ya Jeshi hilo kuanza kutumia namba mpya zenye jina la jeshi hilo la
Magereza.
Comments