AIRTEL YATOA MSAADA WA VITABU VYA SHILINGI MILIONI 9 KWA SHULE ZA SEKONDARI KAGERA
Shule zilizofaidika na msaada wa vitabu hivi ni pamoja na shule za sekondari za Kanyeranyere iliyoko muleba, Kirushya wilayani Ngara pamoja na Nyamigogo iliyoko Biharamuro kagera
Akiongea wakati wa halfa fupi ya kukabidhi vitabu vya masomo ya sayansi na hisabati Afisa elimu wa shule za sekondari mkoani KageraFlorian Kimolo alisema" shule nyingi za sekondari katika mkoa wa Kagera zimekuwa na upungufu mkubwa wa vifaa vya kujifunzia nakufundishia sanjari na uhaba wa vifaa vya maabara na walimu. Kutokana na upungufu wa vitendea kazi katika shule mbalimbali za sekondari hapa nchini tunaomba wadau wa elimu kujitokeza katika kusaidia kulitatua tatizo hilo ili shule hizo ziweze kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Tunashukuru sana Airtel kwa mchango wao katika elimu na katika kuhakikisha tunapata wanafunzi wengi wa masomo ya sayansi na walimuwanapata vitabu vya kutosha katika kufundishia masomo haya na mwisho kupata ufaulu wa kiwango cha juu.
Naye Meneja mauzo wa Airtel katika mikoa ya Kagera na Kigoma Peter Kimaro alisema " Airtel imejipanga kuendeleza ushirikiano na serikaliili kuisaidia wizara ya elimu kufikia malengo waliojiwekea ikiwemo upatikanaji wa vitabu mashule na kuongeza kiwango cha ufaulu. Hadisasa kwa kupitia mradi wa " shule yetu tumeweza kufikia shule nyingi za sekondari nchini. Na nimatumaini yetu vitabu tunavyowakabidhi leovitaleta mabadiliko ya elimu kwa shule hizi na mkoa wa Kagera kwa ujumla.
Naye mkuu wa shule ya sekondari Kanyeranyere iliyoko wilyani Muleba mkoani Kagera alitoa shukurani kwa niaba ya walimu wakuu wa shule za sekondari za kanyeranyere, Kirushya na Nyamigogo na kusema, tunashukuru Airtel kwa kuzikumbuka shule za mkoani Kagera, tunaahidikuvitumia vizuri vitabu hivi ili kuleta ufanisi zaidi na maendeleo ya kitaaluma katika shule zetu.
Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia vitabu mashuleni, zaidi
ya shule 900 za sekondari hapa nchini zimenufaika kupitia kampeni ya
mradi wa kampuni ya simu za mkononi Airtel ujulikanao "Airtel shule
yetu"
Comments