ARSENE WENGER ATAKA WACHEZAJI SOKA WAPIMWE DAMU


LONDON, England
Kauli ya Wenger inakuja kufuatia daktari wa Kihispania Eufemiano Fuentes kufichua kuwa amekuwa na orodha ya wateja wanasoka wanaotumia dawa haramu kama ilivyo kwa waendesha baiskeli wenye kesi juu ya sakata hilo
MFARANSA anayaeinoa Arsenal, Arsene Wenger, ameshauri kuwe na vipimo vya damu kwa wachezaji wa soka na sio mkojo pekee, ili kuondoa tatizo la udanganyifu na matumizi ya dawa zilizopigwa marufuku michezoni.
Wenger amesisitiza umuhimu wa kutumia damu badala ya mkojo, ambapo alisema: “Maofisa wa Kudhibiti Dawa Haramu wa UEFA hawachukui sampuli za damu, wao wanachukua mkojo pekee. Nimeuiliza juu ya hilo mara nyingi, kuna haja ya kubadilika.
“Mara nyingine unaweza kusubiri hadi kwa masaa mawili baada ya mechi kumalizika, hivyo kama watachukua vipimo kwa sampuli za damu inaweza kuleta wepesi na uharaka.
“Natumaini hatuna tatizo kubwa katika utumiaji wa dawa haramu, lakini tutajaribu kujiangalia katika hilo na kuona ni kwa namna gani tunaweza kuingia katika udhibiti.
“UEFA wako tayari kufanya hivyo, lakini unaleta matatizo ya kimaadili na kitabibu kwa sababu kila mmoja anaweza kukubali kupimwa damu na si kila mtu yuko tayari kufanya uchunguzi wa aina hiyo.”
Kauli ya Wenger inakuja kufuatia daktari wa Kihispania Eufemiano Fuentes kufichua kuwa amekuwa na orodha ya wateja wanasoka wanaotumia dawa haramu kama ilivyo kwa waendesha baiskeli wenye kesi juu ya sakata hilo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI