ETO'O ALIGOMA KUJA TANZANIA AKIHOFIA KIFO, AFICHUA SIRI NZITO JINSI MAISHA YAKE YALIVYO SHAKANI


MSHAMBULIAJI Samuel Eto’o amesema viongozi wa soka Cameroonian wanataka afe. 
Nyota huyo wa zamani wa Barcelona na Real Madrid alisema hayo katika mahojiano ya kwenye mtandao aliofanyiwa nyumbani kwao, na kuweka bayana kwamba ameweka ulinzi mkali wa Polisi nyumbani kwake kumlinda.
Nahodha huyo wa Cameroon, ambaye ameshinda Tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika mara nne, amekuwa kwenye mgogoro na Shirikisho la Soka la nchini mwake kwa muda sasa, ingawa mara ya mwisho ilielezwa tofauti zao zimemalizwa. 
Defeated: Samuel Eto'o's Cameroon failed to qualify for the Africa Cup of Nations
Samuel Eto'o na Cameroon walishindwa kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika

Kwa mujibu wa taarifa zilizofikia BIN ZUBEIRY, Eto’o alipozungumza na jarida la Je Wanda alisema: ‘Viongozi wa FCF wanataka kushambulia maisha yangu, wanataka kuniua. 
‘Ninaishi na kundi la walinzi na mmoja analala mbele ya mlango wangu. nafanya hivi siyo kwa sababu wizi, lakini kwa usala wangu.’
Eto’o, ambaye sasa anachezea klabu tajiri, Anzhi Makhachkala ya Urusi, amekuwa akiwashutumu mabosi hao wa FCF kwa kushindwa kuwajibika na kuendekeza rushwa, na kwamba angependa kupewa jezi ya kuchezea kutoka moja kwa moja kwa wasambazaji wa Puma, kuliko chama cha soka. 
Protection: Eto'o says he sleeps with guards outside his room
Eto'o anasema analala walinzi kibao chumbani kwake

Alisema: ‘[Shirikisho] wamebwia fedha zetu kwa muda mrefu kiasi cha kutosha. Badala ya kuongoza soka kwa maslahi yao jumla, wanafikiria maslahi yao tu, kusafiri daraja la kwanza na kufungua akaunti Ulaya.’
Wiki iliyopita, Eto’o na wachezaji wengine 10 waligoma kuja Tanzania kuungana na timu yao ya taifa, Indomitable Lions kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Taifa Stars, wakisingizia majeruhi. Wamekosa tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka huu. 
FCF bado haijajibu chochote kuhusu madai ya Eto'o, ingawa wiki iliyopita, Ofisa mmoja mkubwa kumtuhumu nyota huyo kuvuruga soka kwenye nchi hiyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.