Askari wa kupambana na fujo wa
Misri wamewekwa kwa wingi nje ya ikulu ya rais mjini Cairo baada ya
mapambano ya Ijumaa usiku baina ya wanajeshi na waandamanaji
waliowatupia mabomua ya petroli.
Maandamano hayo ambayo piya yalifanywa katika miji mengine kadha ya Misri, ndio ya karibuni kabisa katika mfulululizo wa maandamano ya kumpinga Rais Mohammed Morsi wa chama cha Muslim Brotherhood.
Upinzani unamlaumu kuwa amepindukia madaraka yake.
Televisheni imeonesha matokeo ya maandamano ya jana usiku - mawe na takataka zimejaa mabara-barani.
Comments