kinana akamilisha ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo wilaya ya kakonko na kibondo mkoani kigoma.


Katibu Mkuu wa CCM-Taifa,Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelekezo mafupi kuhusiana na bwawa la umwagiliaji kutoka kwa Injinia wa maji mkoa wa Kigoma,Elinatha Elisha (haonekani pichani).Kinana amefanya ziara ya kuutembelea mradi huo wa umwagiliaji katika kijiji cha Nyendara,Wilayani Kibondo mkoani Kigoma akiwa ameambatana na wajumbe wake wa chama cha CCM. 
Katibu Mkuu wa CCM-Taifa,Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelekezo mafupi ya mitambo ya umwagiliaji kutoka kwa Injinia wa maji mkoa wa Kigoma,Elinatha Elisha.Kinana amefanya ziara ya kuutembelea mradi huo wa umwagiliaji katika kijiji cha Nyendara,Wilayani Kibondo mkoani Kigoma. 
Sehemu ya mradi wa Bwawa la umwagiliaji,ambalo Katibu Mkuu wa CCM-Taifa,Ndugu Abdulrahman Kinana alitembelea na kujionea maendeleo yake,kwa mujibu wa Injinia kutoka Ofisi ya Umwagiliaji kanda ya Magharibi mkoani Tabora,Bwa.Bahati Balekele alieleza manufaa ya  Bwawa hilo kwa wakazi wa eneo hilo.alisema kuwa litasaidia katika matumizi ya Kilimo cha Umwagiliaji,Matumizi ya mifugo pamoja na matumizi ya majumbani.

Katibu Mkuu wa CCM-Taifa,Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na baadhi ya wanakijiji Nyendara,alipokwenda kukagua mradi wa bwawa la Umwagiliaji la Nyendara
Meneja wa kituo cha uzalishaji Umeme Wilaya ya Kibondo,Damson Lupenza akifafanua jambo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM-Taifa,Ndugu Abdulrahman Kinana na wajumbe wake waliofika eneo hilo kwa ajili kukagua maendeleo ya mradi huo wa Umeme.
Katibu Mkuu wa CCM-Taifa,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa kituo kinachozalisha umeme Wilaya ya Kibondo.
Mmoja wa mafundi wa kituo cha kuzalisha umeme,Omary Mwinyimkuu akitoa maelezo mafupi kwa Katibu Mkuu wa CCM-Taifa,Ndugu Abdulrahman Kinana (pichani kati),alipokwenda kutembelea mradi wa Umeme,kijiji cha Twabangondozi,Wilayani Kibondo akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa ngazi ya juu kichama wilayani humo akiwemo mkuu wa Wilaya,Mh Venance Mwamoto

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.