BULEMBO akikagua gati la kuegemeshea meli linaloendelea kujengwa katika
wilaya ya mafia. Gati hilo ambalo ni muhimu sana kwa wananchi wa wilaya
hiyo linatarajiwa kumalizika mwezi wa tatu mwaka huu. Wengine katika
picha ni viongozi wa CCM.
MWENYEKITI wa Jumuia ya Wazazi tanzania, Abdallah Bulembo akizungumza
na Mkuu wa kituo cha polisi cha wilaya ya Mafia kuhusu malalamiko ya
askari wa usalama barabarani wa kituo chake, aliyetajwa kwa jina moja la
Luka kwamba amekuwa akijihusisha na vitendo vya kuomba na kupokea
rushwa akimtaka afanye utaratibu wa kumuhamisha katika kituo hicho ili
kurudisha heshima ya jeshi hilo kwa wananchi wa wilaya hiyo. Mkuu huyo
wa kituo alimuahidi Bulembo kulifanyia kazi suala hilo. Kushoto ni Mkuu
wa wilaya ya Mafia Sauda Mtondoo.Picha na Mpiga Picha Maalum
Comments