Nigeria 2 Ivory Coast 1


Didier Drogba
Kipindi cha pili kinaelekea ukingoni. Nigeria 2 Ivory Coast 1.
Nigeria ndiyo iliyokuwa ikiongoza kwa kufunga bao kipindi cha kwanza kupitia kwa mchezaji wake Emmanuel Emenike katika dakika ya 45.
Ivory Coast ilisawazisha bao hilo baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Didier Drogba na kumfikia mfungaji Cheick Tiote katika dakika ya 51 na kuunganisjha kwa kichwa mpira huo.
Emmanuel Emenike
Hata hivyo Nigeria ilipata bao lingine la pili katika dakika ya 78 likifungwa na Sunday Mba.
Kikosi cha Ivory Coast ambacho kilionekana kuwa ni bora zaidi katika michuano hii, kimeonekana kuendelea na mkosi wake kama ilivyokuwa mwaka jana wakitolewa katika fainali na Zambia, timu ambayo haikupewa nafasi.
Hata hivyo timu zote zinazidi kushambuliana kwa sababu kufungwa kuna maana ya kuyaaga mashindano haya ya mwaka 2013.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.