Ujumbe wa Rais Barack Obama kwa Wakenya



Rais wa Marekani Barack Obama amewaomba wakenya ambako babake alizaliwa kujiepusha na ghasia pamoja na vitisho katika uchaguzi mkuu unaokuja.
Alituma ujumbe wake kupitia mtandao wa You tube na kuanza ujumbe wake kwa kiswahili.
Alisema uchaguzi ulikuwa fursa nzuri kwa wakenya kuungana kuonyesha kuwa wao sio watu wa makabila bali taifa linaloweza kujivunia.
Uchaguzi mkuu wa Kenya uliokumbwa na utata mwaka 2007 ulisababisha ghasia na vurugu ambapo watu zaidi ya 1,000 waliuawa
Wakenya watapiga kura tarehe 4 mwezi Machi, kumchagua rais na waakilishi wengine, katika uchaguzi mkuu wa kwanza tangu ule uliokumbwa na ghasia.
''Wakenya lazima wakatae vitisho, na ghasia na waweze kuruhusu uchaguzi huru na wa haki. Wakenya lazima wasuluhishe mizozo kwa kupitia mahakamani wala sio kupitia vurugu barabarani,'' alisema Obama
''Lakini cha muhimu ni kuwa wananchi wa Kenya lazima waungane kabla na baada ya uchaguzi kushirikiana kuijenga nchi,'' aliongeza Obama
Babake Obama alizaliwa Kenya na nyanyake wa kambo, angali anaishi katikla kijiji cha Kogelo.
Babake Obama alifariki katika ajali ya barabarabni mwaka 1982.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.